-
Hizbullah ya Iraq: Muqawama utaendelea kulitetea taifa la Palestina kwa roho na mali
Dec 12, 2020 22:17Harakati ya Hizbullah ya Iraq imesema, wafanya mapatano wa Kiarabu wasio na irada hawana uwezo wa kuzifuta haki za taifa la Palestina na ikasisitiza kwamba, muqawama utaendelea kulihami na kulitetea taifa la Palestina kwa roho na mali.
-
Wabunge Iraq waitaka serikali ijibu mapigo kwa kutowapatia viza raia wa Imarati
Nov 27, 2020 08:33Baada serikali ya Imarati kusitisha utoaji viza kwa raia wa Iraq wanaotaka kuingia nchini humo, sambamba na kuwaweka kizuizini katika mazingira ya kutatanisha Wairaqi kadhaa wanaoishi nchini humo, wabunge wa Iraq wameitaka serikali yao isitishe kutoa viza kwa raia wa Imarati pia wanaotaka kuingia nchini humo.
-
Kuondoka askari wa Marekani nchini Iraq; msimamo wa serikali ya Baghdad na makundi ya mapambano
Nov 24, 2020 23:12Katika hali ambayo viongozi wa serikali ya Baghdad wanasema kuwa askari 500 wa Marekani wataanza kutoka katika ardhi ya Iraq miezi miwili ijayo, Sheikh Qais al-Khaz'ali, Katibu Mkuu wa Harakati ya Asaib Ahlul Haq, karibuni hivi alitetea silaha za harakati hiyo ya mapambano ya Kiislamu akisisitiza kuwa muhula wa usitishaji vita na Marekani umekwisha.
-
Bunge la Iraq: Serikali inapasa kuwasilisha matokeo ya uchunguzi kuhusu mauaji ya Kamanda Suleimani
Nov 23, 2020 00:56Kamisheni ya Usalama na Ulinzi ya Bunge la Iraq imeripoti kuwa inaendelea kuishinikiza serikali ya nchi hiyo ili iwasilishe haraka iwezekanavyo matokeo ya uchunguzi kuhusu mauaji ya Kamanda Luteni Jenerali Qassim Suleimani na Abu Mahdi al Muhandis.
-
Ubalozi wa Marekani Iraq ndio pekee duniani unaolindwa kwa mtambo wa makombora ya ulinzi wa anga
Nov 22, 2020 00:42Mbunge wa mrengo wa As-Sadiqun katika bunge la Iraq amesema, ubalozi wa Marekani nchini humo ndio ubalozi pekee duniani unaolindwa kwa mtambo wa makombora ya ulinzi wa anga.
-
Ushirikiano wa genge la kigaidi la ISIS na Marekani wazidi kufichuliwa
Nov 20, 2020 23:04Televisheni moja ya Iraq imesambamba nyaraka mpya zinazoonesha kuweko ushirikiano mkubwa baina ya genge la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) na Shirika la Kijasusi la Marekani, CIA.
-
Mashambulizi ya jeshi la Marekani yameua raia 13,000 Syria na Iraq
Nov 20, 2020 00:09Shirika lisilo la kiserikali la Airwars lenye makao yake mjini London Uingereza limeripoti kuwa, raia wasiopungua 13,000 wa Syria na Iraq wameuawa katika mashambulizi ya muungano unaodaiwa kupambana na magaidi wa Daesh wa Marekani katika kipindi cha miaka sita iliyopita.
-
Hitilafu katika kambi ya Warepublican kuhusu kuondolewa askari wa Marekani Asia Magharibi
Nov 17, 2020 22:53Uamuzi wa Rais Donald Trump wa Marekani wa kuondolewa askari wa nchi hiyo katika eneo la Asia Magharibi hususan Afghanistan na Iraq ambao unatarajiwa kutangazwa katika siku za usoni na iliyokuwa moja ya ahadi muhimu za Trump umekabiliwa na upinzani mkali wa chama chake cha Repulican katika Kongresi ya nchi hiyo.
-
Meja Jenerali Salami: Tutalipiza kisasi cha damu ya kamanda Suleimani kwa waliomuua
Nov 16, 2020 04:29Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesisitiza tena akisema: "Tutalipiza kisasi cha damu ya kamanda shahidi Qassim Suleimani kwa waliomuua."
-
Mbunge wa Iraq: Muswada wa kutimuliwa wanajeshi wa Marekani, utekelezwe haraka
Nov 15, 2020 04:37Mjumbe mmoja wa Kamisheni ya Usalama na Ulinzi ya Bunge la Iraq amesisitiza kwamba, hakutakuwa na tofauti yoyote kubadilishwa sura ya rais wa Marekani, lililo muhimu kwa Iraq ni kutekelezwa muswada uliopasishwa na bunge la nchi hiyo wa kutimuliwa wanajeshi wa Marekani nchini Iraq.