-
Waziri wa Ulinzi wa Marekani: Vita vya mwaka 2003 ndio sababu ya matatizo ya leo ya Iraq
May 29, 2020 06:28Waziri wa zamani wa Ulinzi wa Marekani amesema kuwa vita vya mwaka 2003 vya Marekani nchini Iraq ndio chanzo kikuu cha matatizo ya sasa ya nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Jeshi la Iraq lamuua kiongozi wa ISIS nchini Syria
May 29, 2020 01:46Televisheni ya al Mayadeen imeripoti kuwa, kiongozi mmoja mkubwa wa genge la kigaidi la Daesh (ISIS) ameuawa katika shambulio la anga lililofanywa na jeshi la Iraq katika maficho ya magaidi hao huko Deir ez-Zor, Syria.
-
Iraq: Hatuna haja na wageni katika kupambana na magaidi wa ISIS
May 27, 2020 21:53Msemaji wa vikosi vya ulinzi vya Iraq amesema, nchi yake ina uwezo wa kutosha wa kupambana na kuwamaliza magaidi wa Daesh (ISIS) hivyo haina haja na msaada wa wanajeshi kutoka nje.
-
Kiongozi wa ISIS nchini Iraq auawa katika shambulizi la anga
May 26, 2020 23:14Kikosi cha Kupambana na Ugaidi cha Jeshi la Iraq kimetangaza habari ya kuangamizwa kinara wa kundi la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) nchini humo, Mu'taz al-Jubouri katika shambulizi la anga.
-
Kufichuliwa kashfa ya Saudia ya kutuma maelfu ya magaidi nchini Iraq
May 25, 2020 00:02Kusambazwa faili la sauti katika mitandao ya kijamii kumepelekea kufichuliwa kashfa ya Saudi Arabia kutuma maelfu ya magaidi wa nchi hiyo kwenda Iraq katika miaka ya hivi karibuni.
-
Bunge la Iraq lataka kanali ya televisheni ya MBC mali ya Saudi Arabia ipigwe kufuli kwa kuwadhalilisha shakhsia wa nchi hiyo
May 15, 2020 21:58Kamisheni ya Mahusiano na Vyombo vya Habari ya Bunge la Iraq imetaka kufungwa kanali ya televisheni ya Saudi Arabia ya MBC, kufuatia kanali hiyo kumvunjia heshima Naibu Mkuu wa Harakati ya Wananchi ya Hashdu sh-Sha'abi ya nchi hiyo.
-
Harakati ya Asa'ib Ahl al-Haq ya Iraq: Tunafuatilia kwa umakini harakati zote za Marekani
May 13, 2020 23:23Msemaji wa Harakati ya Muqawama ya Asa'ib Ahl al-Haq ya nchini Iraq amesisitiza kwamba Wamarekani na vibaraka wao wanatakiwa kufahamu kwamba macho ya muqawama daima yanafuatilia harakati zao kwa umakini mkubwa.
-
Waziri Mkuu wa Iraq apongeza uungaji mkono wa Iran katika vita dhidi ya ISIS
May 10, 2020 19:53Waziri Mkuu mpya wa Iraq ameipongeza na kuishukuru Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa msaada na uungaji mkono wake katika mapambano dhidi ya kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh (ISIS).
-
Kupata ridhaa ya Bunge serikali mpya ya Iraq; mwisho wa mkwamo wa kisiasa wa miezi mitano
May 07, 2020 07:04Baada ya miezi mitano ya mkwamo wa kisiasa nchini Iraq, hatimaye Bunge la nchi hiyo limeidhinisha Baraza la Mawaziri la Waziri Mkuu Mustafa al-Kadhimi.
-
Operesheni kali dhidi ya mabaki ya wanachama wa Daesh (ISIS) yaanza nchini Iraq
May 05, 2020 06:50Msemaji wa Kamandi Kuu ya Jeshi la Iraq ameelezea amri ya Adil Abdul-Mahdi, Waziri Mkuu wa Iraq ya kuanzishwa operesheni kali dhidi ya mabaki ya wanachama wa kundi la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) nchini humo.