-
Hamas: Mwisho wa Abu Shabab ndio hatima isiyoepukika ya kila msaliti
Dec 05, 2025 10:50Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imeonya kwamba mauaji ya mshirika wa Israel na kiongozi wa genge lenye uhusiano na Daesh, Yasser Abu Shabab, ni hatima isiyoepukika ya kila mtu anayechagua kulisaliti taifa na nchi yake na kushirikiana na utawala ghasibu wa Israel.
-
Yasser Abu Shabab, mshirika wa Israel na msaliti wa Wapalestina wa Ghaza aripotiwa kuuawa
Dec 05, 2025 06:55Yasser Abu Shabab, mshirika wa kijeshi wa utawala wa kizayuni wa Israel mwenye uhusiano pia na kundi la kigaidi la DAESH (ISIS), maarufu kwa kuongoza uporaji wa misaada ya kibinadamu katika Ukanda wa Ghaza na kwa kuwalenga kwa kuwaua raia wa Palestina, ameripotiwa kuuawa katika eneo hilo.
-
Spika wa Bunge: Iran iko wazi kwa diplomasia lakini usalama wa taifa na nguvu ya ulinzi haviwezi kujadiliwa
Dec 05, 2025 02:58Spika wa Bunge la Iran, Mohammad-Baqer Qalibaf amesema ingawa Iran iko wazi kwa diplomasia, lakini haitalegeza kamba katika suala la usalama wa taifa na nguvu zake za ulinzi.
-
Azimio la UN: Israel inaikalia "kinyume cha sheria" Miinuko ya Golan ya Syria, iondoke kikamilifu
Dec 03, 2025 10:54Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepitisha azimio linalotangaza kuwa, kuendelea Israel kuikalia kwa mabavu na kuiunganisha na upande wake Miinuko ya Golan ya Syria ni "kinyume cha sheria" na limeutaka utawala huo uondoke kikamilifu katika eneo hilo hadi kwenye mstari wa mpaka wa Juni 4, 1967.
-
Kampeni ya 'Komboa Mateka Wapalestina' walioko kwenye magereza ya Israel yazidi kupamba moto
Dec 01, 2025 05:45Maelfu ya waandamanaji jana Jumamosi walimiminika kwenye eneo la katikati mwa mji mkuu wa Uingereza, London katika maandamano ambayo ni sehemu ya kampeni ya "Komboa Mateka Wapalestina", wakitaka kuachiliwa huru Wapalestina zaidi ya 9,100 wanaoshikiliwa katika magereza ya kutisha ya utawala wa kizayuni wa Israel, wakiwemo zaidi ya wanawake na watoto 450.
-
Maelfu ya Waisrael wafurika kwenye ubalozi wa Ureno Tel Aviv kuomba uraia wa nchi hiyo
Dec 01, 2025 05:44Tovuti ya gazeti la kizayuni la Times of Israel imeripoti kuwa, maelfu ya Waisrael wamepanga foleni ndefu mbele ya ubalozi wa Ureno mjini Tel Aviv kwa lengo la kuomba uraia wa nchi hiyo.
-
Changamoto mbili zinazoutesa utawala wa Kizayuni baada ya vita vya siku 12 dhidi ya Iran
Nov 30, 2025 09:49Katika ripoti yake ya hivi karibuni kabisa, tovuti ya Middle East Eye imefanya uchunguzi kuhusu changamoto zinazoikabili Tel Aviv baada ya vita vya kivamizi na kichokozi vya siku 12 ilivyovianzisha dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Amnesty International: Israel inaendelea kufanya mauaji ya kimbari Ghaza
Nov 29, 2025 11:14Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limetangaza kuwa, utawala wa kizayuni wa Israel "unaendelea bila kusita kufanya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina huko Ghaza, licha ya usitishaji mapigano" ulioanza kutekelezwa tarehe 10 Oktoba.
-
Baraza la Waislamu Ufaransa latoa wito wa kufanyika uchunguzi kuhusu ujasusi dhidi ya Waislamu kwa niaba ya Israel
Nov 29, 2025 03:24Baraza la Waislamu la Ufaransa limetoa wito kwa serikali kuanzisha uchunguzi kuhusu madai kwamba watu wawili walikusanya taarifa kuhusu Waislamu nchini Ufaransa na kuzikabidhi kwa shirika la ujasusi la Israel.
-
Israel yatumia mfumo wa akili mnemba (AI) kufuatilia mitandao ya kijamii ya wanajeshi, ili kuzuia ushahidi wa uhalifu wa kivita
Nov 28, 2025 02:59Jeshi la Israel limezindua mradi mkubwa wa akili mnemba (AI), unaojulikana kama Morpheus, ili kuzuia askari wake kuchapisha ushahidi wa uhalifu wa kivita uliofanyika huko Gaza kwenye mitandao ya kijamii.