-
Italia yaanzisha uchunguzi dhidi ya Ben-Gvir kuhusu unyanyasaji wa wanaharakati wa Global Sumud Flotilla
Jun 10, 2026 03:59Waendesha mashtaka wa Italia wameanzisha uchunguzi dhidi ya Waziri wa Usalama wa Israel mwenye msimamo mkali wa mrengo wa kulia, Itamar Ben-Gvir kuhusu mateso, unyanyasaji na utekaji nyara wa wanaharakati walioshiriki katika msafara wa Global Sumud Flotilla wa kupeleka misaada ya kibinadamu kwa watu wa Gaza, mwezi uliopita.
-
Hamas yaonya kuhusu ongezeko la ubomoaji wa majengo Ukingo wa Magharibi, yataka hatua za kimataifa zichukuliwe dhidi ya Israel
Jun 10, 2026 03:55Harakati ya Hamas imeonya kuhusu ongezeko la shughuli za ubomoaji wa nyumba na majengo ya Wapalestina unaofanywa na Israel katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu, ikiwa ni pamoja na al-Khalil, ikitaja vitendo hivyo kuwa ni ukiukaji wa sheria za kimataifa.
-
Guterres: Wafanyakazi 80 wa Umoja wa Mataifa waliuawa mwaka jana huko Gaza
Jun 09, 2026 11:46Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, ametangaza kwamba wafanyakazi 136 wa shirika hilo la kimataifa waliuawa wakitekeleza majukumu yao katika mwaka uliopita, wakiwemo wafanyakazi 80 waliokuwa wakifanya kazi katika Ukanda wa Gaza huko Palestina.
-
Papa Leo XIV : Uvamizi wa kijeshi wa Marekani na Israel dhidi ya Iran 'sio vita vya haki'
Jun 07, 2026 03:44Kiongozi wa kanisa katoliki Dunia, Papa Leo XIV amesema uchokozi wa kijeshi wa Marekani na Israel dhidi ya Iran haukuwa "vita vya haki", akisisitiza kwamba itikadi hiyo ya karne nyingi haiendani na uhalisia wa vita vya kisasa.
-
WFP: Vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran vinasukuma mamilioni kukumbwa na njaa Afrika
Jun 06, 2026 03:11Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limeonya kuwa vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran vinawasukuma mamilioni ya watu duniani kuingia katika hali ya njaa huku bara Afrika likionekana kuathirika zaidi.
-
Foreign Policy: Chuki dhidi ya Wakristo imeongezeka huko Israel
Jun 04, 2026 03:12Uchunguzi uliofanywa na baadhi ya vyombo vya habari umebaini kuwa chuki na hujuma dhidi ya Wakristo vimeongezeka huko Israel.
-
Israel yafuta mpango wa kushambulia Beirut baada ya onyo kali la Iran
Jun 02, 2026 09:12Utawala wa Israel umeachana na mpango wake wa kufanya mashambulizi makali ya ya kijeshi dhidi ya mji mkuu wa Lebanon, Beirut. Haya yameelezwa siku ya Jumatatu na Rais wa Marekani, Donald Trump, kufuatia onyo kali kutoka kwa Iran kwamba haitavumilia wimbi jipya la uvamizi dhidi ya Beirut, hatua ambayo ingekiuka makubaliano ya kusitisha vita kati ya Iran na Marekani.
-
Mwanasiasa wa Ujerumani: EU ni mshirika katika ugaidi wa kimfumo wa Israel
Jun 01, 2026 02:55Mwanasiasa wa Ujerumani na mbunge wa zamani wa bunge la nchi hiyo amekosoa sera za utawala wa Kizayuni wa Israel na kusema: "Walowezi wa Kizayuni wanafanya ugaidi wa kimfumo dhidi ya Wapalestina, na serikali ya Ujerumani na Umoja wa Ulaya wanashiriki katika uhalifu huo kwa kunyamaza kimya."
-
Waziri wa Israeli Ben-Gvir amhimiza Netanyahu 'kusawazisha vitongoji vya Beirut na ardhi'
May 31, 2026 12:48Waziri anayejiita wa usalama wa Israel, Itamar Ben-Gvir, amemtaka Waziri Mkuu wa utawaka huo katili, Benjamin Netanyahu, kusawazisha na ardhi vitongoji vya mji mkuu wa Lebanon, Beirut huku utawala huo ukizidisha mashambulizi yake dhidi ya nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Iran yalaani ukiukaji wa Marekani wa makubaliano ya amani, yahimiza UN kuingilia kati
May 29, 2026 03:18Iran imelaani vikali vitisho vya mara kwa mara vya Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu na ukiukaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyosimamisha vita haramu vya hivi karibun, ikiuhimiza Umoja wa Mataifa kuingilia kati.