-
'Hakuna vita vya masaa 2', yasema Iran ikiapa kutoa jibu la haraka kwa uchokozi wa US au Israel
Jan 30, 2026 04:17Jeshi la Iran limetoa onyo kali kwamba kitendo chochote kipya cha uchokozi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu kitakabiliwa na jibu kali na la haraka, likisisitiza kwamba uzoefu na tajiriba ya vita vya Juni vimebadilisha kimsingi muelekeo wa kijeshi wa Iran na kanuni zake za makabiliano.
-
Afisa mwandamizi wa jeshi la Israel: Iran ni dola moja kuu kwa makombora duniani
Jan 30, 2026 04:17Kamanda wa zamani wa mitambo ya ulinzi wa anga wa utawala wa kizayuni wa Israel ameielezea Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuwa ni moja ya madola makuu duniani kwa upande wa masuala ya anga na ulimwengu wa makombora, na akasema, Tehran itailenga Tel Aviv iwapo kutakuwa na shambulio lolote litakalofanywa na Marekani dhidi yake.
-
Je, Tel Aviv inalenga kuizingira kimkakati Misri katika Bahari Nyekundu?
Jan 28, 2026 23:54Misri, katika kujibu kuongezeka kwa ushawishi na uingiliaji wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika Pembe ya Afrika, imeimarisha uwepo wake wa kijeshi nchini Somalia.
-
Mwanamke Muisraeli ashtuka kujiona kwenye orodha ya 'waliofariki' kwenye machafuko ya Iran
Jan 27, 2026 03:08Kijana wa kike wa kiisraeli aitwaye Noya Zion ameshtuka baada ya kuona picha yake inaonyeshwa kwenye televisheni ya taifa ya Israel kama mmoja wa watu waliouawa katika maandamano nchini Iran, mkasa ambao umezidi kudhihirisha jinsi utawala huo wa kizayuni unavyosambaza habari feki na za uwongo kuhusu machafuko ya hivi karibuni nchini Iran na namna serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ilivyokabiliana nayo.
-
Iran: Tutatoa jibu la 'kujutisha' kwa uchokozi wowote wa maadui
Jan 26, 2026 08:49Iran imeonya kwamba, Jamhuri ya Kiislamu itatoa "jibu la kujutisha" kwa kitendo chochote cha uchokozi, ikisisitiza kwamba taifa hili sasa lina uwezo mkubwa zaidi wa kijeshi kuliko hapo awali.
-
Iran yazifungulia mashitaka US, Israel kwa kuunga mkono ugaidi
Jan 26, 2026 06:46Iran imewasilisha malalamiko ya kisheria na jinai katika majukwaa ya kimataifa dhidi ya Marekani, utawala wa Kizayuni wa Israel, na makundi kadhaa ya kigaidi kwa kuunga mkono na kufadhili vitendo vya ugaidi na uhaini dhidi ya usalama wa taifa wa Iran.
-
Katika mazungumzo na US, Misri yahimiza Israel iondoke Ghaza, ifungue tena kivuko cha Rafah
Jan 26, 2026 00:20Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri Badr Abdelatty ametoa wito kwa utawala wa kizayuni wa Israel kujiondoa katika Ukanda wa Ghaza na kufungua tena kivuko cha mpakani cha Rafah kuliingana na makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyoanza kutekelezwa Oktoba mwaka jana.
-
Shambulio la droni la Israel laua watoto 2 Gaza
Jan 25, 2026 03:46Watoto wawili wameuawa shahidi katika shambulio la Israel kaskazini mwa Ukanda wa Gaza, katika ukiukaji wa hivi karibuni wa makubaliano ya kusitisha mapigano baina ya utawala huo katili na Harakati ya Muqawama ya Hamas katika eneo hilo la Wapalestina linalokaliwa kwa mabavu.
-
Albanese: Israel ifukuzwe UN kwa kubomoa makao makuu ya UNRWA
Jan 24, 2026 07:03Ripota Maalum wa Umoja wa Mataifa katika maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu ameilaani Israel kwa kubomoa makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Palestina (UNRWA) katika mji wa Baitul Muqaddas Mashariki unaokaliwa kwa mabavu, na kutaka kusimamishiwa unachama utawala huo wa Kizayuni katika Umoja wa Mataifa.
-
B’Tselem: Wapalestina wasiopungua 84 wameuawa kwenye kambi za mateso za Israel
Jan 21, 2026 07:09Mfumo wa magereza wa utawala wa kizayuni wa Israel umekuwa "mtandao wa kambi za mateso" unaowalenga Wapalestina. Hayo yameelezwa katika ripoti mpya ya uchunguzi uliofanywa na asasi ya kutetea haki za binadamu ya B'Tselem.