-
Rais Rouhani: Kama Marekani inaogopa moto basi haipaswi kuwasha muale
Jul 03, 2019 08:31Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa makubaliano ya nyuklia ya JCPOA yana manufaa kwa mataifa yote, eneo la Mashariki ya Kati na dunia nzima na kuongeza kuwa, Kama Marekani inaogopa moto haipaswi kuwasha muale na itekeleze maazimio ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Hatua mpya ya Iran katika kujibu ukiukaji ahadi wa madola ya Ulaya; Iran yavuka kiwango cha kilo 300 za urani iliyorutubishwa
Jul 02, 2019 22:04Kwa mujibu wa kifungu nambari 36 cha makubaliano ya nyuklia ya Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji JCPOA, Iran imevuka kiwango cha kilo 300 za urani iliyorutubishwa.
-
Balozi wa Iran UN: INSTEX bila mtaji ni sawa na gari zuri bila mafuta
Jun 30, 2019 03:09Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema mfumo maalumu wa mabadilishano ya fedha kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Umoja wa Ulaya (INSTEX) ni sawa na gari zuri ambalo halina mafuta.
-
Taarifa ya mwisho ya kikao cha kamisheni ya JCPOA yatolewa Vienna
Jun 29, 2019 12:24Kamisheni ya makubaliano ya nyuklia ya JCPOA imetoa taarifa mwishoni mwa kikao chake huko Vienna na kutangaza kuwa wanachama wa JCPOA wanafanya jitihada za kufungua mfumo maalumu wa mabadilishano ya fedha kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Umoja wa Ulaya, Instex mbele ya wadau wa masuala ya uchumi wa nchi nyingine.
-
Kikao cha Vienna na 'JCPOA'; udharura wa kuwa huru Ulaya kivitendo
Jun 29, 2019 02:17Sambamba na kukaribia kumalizika kwa muhula wa siku 60 uliotolewa na Iran kwa nchi za Ulaya ili zichukue hatua za kivitendo zenye lengo la kulinda mapatano ya nyuklia ya JCPOA, udiplomasia wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran unafuatilia maslahi yake ya kitaifa bila kujali mashinikizo ya kisiasa na kiuchumi.
-
Misimamo ya kimasharti ya troika ya Ulaya kuhusu JCPOA
Jun 26, 2019 02:17Huku muda uliowekwa na Iran wa kuongeza kiwango cha kutochunga ahadi zake ndani ya mapatano ya nyuklia ya JCPOA kutokana na upande wa pili wa mapatano hayo kutotekeleza kabisa ahadi zao ukikaribia, troika ya Ulaya yaani nchi tatu za Ujerumani, Ufaransa na Uingereza zimeanzisha harakati za kidiplomasia na kipropaganda za kujaribu kuizuia Iran isichukue hatua zaidi za kupunguza utekelezaji wa ahadi zake.
-
Katibu Mkuu wa UN: Iran ingali imefungamana na JCPOA
Jun 21, 2019 06:59Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa mara nyingine tena amesisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imefungamana na makubaliano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Federica Mogherini asisitiza kulindwa makubaliano ya JCPOA
Jun 20, 2019 03:03Mkuu wa Siasa za Nje wa Umoja wa Ulaya amesisitiza kulindwa makubaliano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Iran: Hatutarefusha muhula wa siku 60 wa EU kufungamana na JCPOA
Jun 19, 2019 08:15Msemaji wa Taasisi ya Nishati ya Atomiki ya Iran (AEOI) amesema muda wa siku 60 ambao Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iliupa Umoja wa Ulaya uwe umetekeleza ahadi zake za kufungamana na makubaliano ya nyuklia ya JCPOA hautarefushwa.
-
Njia za utatuzi za Rais Vladmir Putin kwa ajili ya mapatano ya JCPOA
Jun 17, 2019 00:04Hatua ya Marekani ya kujiondoa kwenye mapatano ya nyuklia ya JCPOA mwezi Mei mwaka jana na pia ukiukaji wa ahadi wa mara kwa mara wa Umoja wa Ulaya ambao umeshindwa kulinda mapatano hayo kupitia kuanzisha mfumo utakaosaidia kupunguza athari hasi za vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran, ni mambo yaliyoyaweka katika hali mbaya mapatano hayo.