Pars Today
Wataalamu wa masuala ya ulinzi kutoka nchi za Afrika Mashariki wanakutana nchini Uganda kujadili njia za kuimarisha amani na usalama kieneo.
Hatua ya Kenya kutoteua wabunge wake wa Bunge la Afrika Mashariki EALA hadi sasa imechelewesha kuanza vikao vya chombo hicho cha kieneo.
Bunge la Afrika Mashariki EALA limesema karibuni hivi litaanza kuchunguza kwa shabaha ya kuupatia ufumbuzi mzozo na uhasama kati ya nchi jirani za Rwanda na Burundi.
Bunge la Afrika Mashariki EALA limefanya kikao maalumu asubuhi ya leo mjini Arusha Tanzania, kwa ajili ya kumuenzi Hafsa Mossi, mwakilishi wa Burundi katika bunge hilo la kieneo ambaye aliuawa wiki jana mjini Bujumbura.
Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) imesema inaunga mkono kufanyika duru ya pili ya mazungumo kati ya serikali ya Burundi na wapinzani.
Bunge la Afrika Mashariki EALA linaandaa muswada ambao ukipasishwa na kuwa sheria, utamaduni wa kuwakeketa mabinti na wanawake utapigwa marufuku katika nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC.
Bunge la Afrika Mashariki EALA limeanza vikao vyake mjini Arusha nchini Tanzania hii leo, huku mjadala kuhusu bajeti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC ikiwa moja ya ajenda kuu katika vikao hivyo.
Ni rasmi sasa Sudan Kusini ni nchi mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC. Hii ni baada ya Rais Salva Kiir wa nchi hiyo kusaini mkataba unaorasimisha nchi hiyo kujiunga na EAC katika mji mkuu wa kibiashara wa Tanzania, Dar es Salaam.
Jumuiya ya Afrika Mashariki ,EAC, inakaribia kuunda jeshi la pamoja kwa lengo la kulinda taasisi muhimu za kiuchumi za nchi wanachama.