Nchi za Afrika Mashariki kuunda Jeshi la Pamoja
(last modified Sat, 26 Mar 2016 01:40:55 GMT )
Mar 26, 2016 01:40 UTC
  • Nchi za Afrika Mashariki kuunda Jeshi la Pamoja

Jumuiya ya Afrika Mashariki ,EAC, inakaribia kuunda jeshi la pamoja kwa lengo la kulinda taasisi muhimu za kiuchumi za nchi wanachama.

Hayo yamebainika wakati wa mafunzo ya pamoja mjini Nairobi ya wanajeshi 300 kutoka Kenya, Uganda, Tanzania, Burundi na Rwanda.

Kamanda wa Majeshi ya Kenya Jenerali Samson Mwathethe amesema kikosi hicho cha pamoja ni muhimu kwa kuzingatia matarajio makubwa ya ustawi wa kiuchumi Uganda na Kenya kutokana na uzalishaji mafuta na gesi asilia Tanzania.

Akizungumza Ijumaa wakati wa mazoezi hayo Jenerali Mwatheteh amesema, “Shirikisho limeanza kupata muundo wake hatua kwa hatua kama ilivyopangwa na nchi zote za EAC ikiwemo Sudan Kusini. Eneo hili lina ukubwa wa mita mraba milioni 2.4 na idadi ya watu milioni 170. Nchi zote wanachama zinafungamana na udumishwaji amani na usalama katika eneo.”

Mkuu wa Jeshi la Kenya amesema ugaidi ni tishio kubwa zaidi la usalama katika eneo na hivyo nchi zote zinapaswa kushirikiana. Akizungumza katika hafla hiyo Waziri wa Ulinzi wa Kenya Raychelle Omamo amesema mafunzo hayo ya maafisa wa kijeshi ni katika fremu ya ushirikiano wa kiulinzi baina ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki. Aidha amesema vikosi vya usalama vinapaswa kufahami mbinu za makundi ya kigaidi yanayolenga kuvuruga uchumi wa eneo hilo.

 

Tags