-
Trump: Huenda kiongozi wa Korea Kaskazini akapatwa na hatima kama ya Gaddafi
May 19, 2018 04:13Rais Donald Trump wa Marekani amemuonya kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un kuwa huenda akapatwa na hatima kama iliyomfika kiongozi wa zamani wa Libya, Kanali Muammar Gaddafi, iwapo Pyongyang haitaachana na mradi wake wa silaha za nyuklia.
-
Onyo la Korea Kaskazini kwa Marekani, lailazimisha Washington kurejea nyuma
May 18, 2018 03:53Kufuatia onyo kali la Korea Kaskazini la kutaka kuvunja kikao tarajiwa kati ya kiongozi wa nchi hiyo na Rais wa Marekani hapo tarehe 12 Juni mwaka huu, hatimaye Washington imelazimika kutangaza kwamba ndege za kivita zenye kubeba mabomu ya nyuklia hazitashirki katika maneva ya pamoja ya anga ya nchi hiyo na Korea Kusini.
-
Onyo la Korea Kaskazini kwa Marekani
May 17, 2018 07:52Katika radiamali ya matamshi ya viongozi wa Marekani dhidi ya Korea Kaskazini na kadhalika maneva ya anga ya kijeshi kati ya Marekani na Korea Kusini, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Korea Kaskazini ametahadharisha kwamba, iwapo Washington itaendeleza mashinikizo yake dhidi ya Pyongyang kuhusu mpango wake wa nyuklia, basi nchi hiyo italazimika kuangalia upya kikao tarajiwa kati ya Trump na Kim Jong-un.
-
Korea Kaskazini yatishia kufuta mkutano wake na Marekani
May 16, 2018 07:19Korea Kaskazini imetishia kufuta mkutano kati ya kiongozi wake, Kim Jong-un na Rais Donald Trump wa Marekani, kutokana na kile inachodai kuwa ni chokochoko za Washington na Korea Kusini dhidi yake.
-
Korea Kaskazini yawaalika waandishi wa habari wa Korea Kusini kuzuru maeneo yake ya nyuklia
May 16, 2018 02:40Wizara ya Umoja ya Korea Kusini imetangaza kwamba, serikali ya Korea Kaskazini imewataka waandishi wa habari wa Korea Kusini kutembelea na kuangalia mwenendo wa kufungwa maeneo ya kufanyia majaribio ya silaha za nyuklia ya nchi hiyo jirani.
-
Korea Kusini yashangazwa na madai ya Japan kwamba inaitumia Korea Kaskazini mafuta
May 14, 2018 13:59Serikali ya Korea Kusini sambamba na kukanusha madai ya Japan kwamba, inatuma mafuta kwenda Korea Kaskazini kwa siri, imesema kuwa Seoul imefungamana vilivyo na vikwazo vya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa dhidi ya Pyongyang.
-
Manuva ya majeshi ya anga ya Marekani na Korea Kusini katika Peninsula ya Korea
May 11, 2018 14:04Manuva makubwa ya vikosi vya anga vya majeshi ya Marekani na Korea Kusini yameanza leo katika Peninsula ya Korea kwa kisingizio cha kuimarisha uwezo wa kushambulia wa nchi hizo mbili.
-
Korea Kaskazini: Marekani inachafua anga ya mazungumzo kwa kueneza uwongo
May 06, 2018 07:32Wiki chache kabla ya kufanyika mazungumzo yanayosubiriwa kwa shauku kuu kati ya Rais Donald Trump wa Marekani na kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un, Pyongyang imekosoa vikali kile ilichokitaja kama upotoshaji wa makusudi wa Washington, kwamba sera za Trump za kushadidisha vikwazo na mashinikizo ya kisiasa dhidi ya nchi hiyo ndizo zilizopelekea Korea Kaskazini kukubali kwenda katika meza ya mazungumzo.
-
Hatimaye Korea Kaskazini yakubali kuangamiza makombora yake ya balestiki
May 03, 2018 14:31Serikali ya Korea Kaskazini sambamba na kukubali kuangamiza makombora yake ya kutoka bara hadi bara ya balestiki, imekubali pia kutumwa wataalamu wa kimataifa kwenda kukagua taasisi za nyuklia za nchi hiyo.
-
Korea ya Kaskazini yakadhibisha madai ya Marekani
May 03, 2018 07:48Ofisi ya Uwakilishi ya Korea ya Kaskazini katika Umoja wa Mataifa imekadhibisha tuhuama za Marekani dhidi ya Pyong Yang kuhusu kuhakiwa vituo vya taarifa vya kamati za vikwazo za Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.