-
Korea Kaskazini yavurumisha makombora ya balistiki
Aug 26, 2017 07:01Korea Kaskazini imevurumisha makombora matatu ya masafa mafupi ya balistiki kuelekea pwani yake ya kaskazini.
-
Korea Kaskazini: Chokochoko za Marekani zikiongezeka, tutaishambulia bila huruma
Aug 20, 2017 16:30Kwa mara nyingine serikali ya Korea Kaskazini imetoa onyo kali kwa Marekani kwa kusema kuwa, ikiwa siasa za uhasama na kupenda kujitanua dhidi ya Pyongyang zitaendelea na hatimaye kuisukuma nchi hiyo kuingia katika vita vya nyuklia, basi Washington itakabiliwa na mashambulizi makali.
-
Mwanastratijia wa Trump: Mgogoro wa Korea Kaskazini hauna njia ya utatuzi wa kijeshi
Aug 18, 2017 04:06Mwanastratijia wa ngazi ya juu wa ikulu ya Marekani (White House) ametoa matamshi yanayopingana na vitisho vya Rais Donald Trump wa nchi hiyo dhidi ya Pyongyang na kusema kuwa, suala la Korea Kaskazini halina njia ya utatuzi wa kijeshi.
-
Katibu Mkuu wa UN akerwa na vita vya maneno kati ya US na Korea Kaskazini
Aug 17, 2017 07:42Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameeleza wasiwasi wake kuhusu kushtadi vita vya maneno kati ya Marekani na Korea Kaskazini na kusema kuwa, kuna haja ya pande mbili hizo kukumbatia diplomasia.
-
Korea Kaskazini: Sharti la kutoshambuliwa kisiwa cha Guam ni Marekani kusitisha chokochoko zake Korea
Aug 16, 2017 14:12Kim Jong-un, Kiongozi wa Korea Kaskazini amesema kuwa, sharti la kusitishwa mashambulizi ya makombora dhidi ya kisiwa cha Guam cha Marekani ni Washington kuhitimisha mivutano katika Peninsula ya Korea.
-
Kim Jong-un alitaka jeshi la Korea Kaskazini kujiweka tayari kwa ajili ya kukishambulia kisiwa cha Guam
Aug 15, 2017 08:10Kim Jong-un, Kiongozi wa Korea Kaskazini amelitaka jeshi la nchi hiyo kujiweka tayari kwa ajili ya kufanya mashambulizi ya makombora dhidi ya kisiwa cha Guam kinachodhibitiwa na Marekani.
-
Korea Kaskazini: Njia pekee ya kuzuia vita katika eneo ni Seoul kuzuia chokochoko za Marekani
Aug 14, 2017 03:41Serikali ya Korea Kaskazini imekosoa mazungumzo ya simu ya Rais Moon Jae-in wa Korea Kusini na Rais Donald Trump wa Marekani yaliyofanyika hivi karibuni na kusema kuwa mazungumzo hayo hayawezi kusaidia kumaliza mgogoro uliopo.
-
Onyo la China juu ya uwezekano wa Marekani kuishambulia Korea Kaskazini
Aug 14, 2017 03:33Gazeti moja muhimu la chama tawala nchini China limeionya Marekani na Korea Kusini juu ya vitisho vyao vya kutaka kuishambulia kijeshi Korea Kaskazini na kusema kuwa, ikiwa maslahi ya China yataingia hatarini kwa vita hivyo tarajiwa, basi bila shaka yoyote nayo itakabiliana na nchi hizo.
-
Mamilioni ya wapiganaji wa kujitolea Korea Kaskazini wajiweka tayari kupambana na Marekani
Aug 13, 2017 03:48Vyombo vya habari nchini Korea Kaskazini vimeripoti kwamba karibu watu milioni 3.5 wa kujitolea wametangaza utayarifu wao kwa ajili ya kupambana na Marekani vitani.
-
Indhari ya Ujerumani na Russia kuhusu hatari ya kutokea vita kati ya Marekani na Korea Kaskazini
Aug 12, 2017 13:32Kuongezeka mivutano na kutoleana kauli za vitisho viongozi wa Marekani na Korea Kaskazini kumeitia wasiwasi mkubwa jamii ya kimataifa juu ya uwezekano wa kutokea vita katika eneo la Mashariki mwa Asia.