-
Kushadidi vita nchini Libya katika kivuli cha virusi vya Corona
Apr 14, 2020 11:13Licha ya kuibuka virusi vya Corona na kuenea kote ulimwenguni na hilo kupelekea kusitishwa vita na mapigano katika maeneo mengi ya dunia, lakini nchini Libya kwa sasa vita vimeshika kasi.
-
Vikosi vya serikali ya Libya vyakomboa miji minane iliyokuwa ikishikiliwa na wapiganaji wa Haftar
Apr 14, 2020 07:48Serikali ya Maafikiano ya Kitaifa ya Libya (GNA) imetangaza kuwa vikosi vyake vimekomboa miji minane iliyokuwa ikidhibitiwa na wapiganaji watiifu kwa jenerali muasi Khalifa Haftar.
-
Wanamgambo 1,500 wa Kisyria wawasili Libya kushirikiana na Haftar
Apr 13, 2020 10:05Vikosi vya jeshi la Khalifa Haftar vimetangaza kuwa wanamgambo 1,500 wa Kisyria wamewasili Tripoli wakisaidiwa na Uturuki.
-
UAE yanunua mfumo wa makombora wa Israel na kuwapa wapiganaji wa Haftar
Apr 13, 2020 03:38Umoja wa Falme za Kiarabu umenunua mfumo wa kisasa wa makombora kutoka utawala wa Kizayuni wa Israel, kwa ajili ya kuwapa wanamgambo wa kundi linalojiita Jeshi la Taifa la Libya (LNA) linaloongozwa na jenerali muasi Khalifa Haftar.
-
Mapigano yaendelea kushuhudiwa Libya baina ya vikosi vya serikali ya Fayez al-Sarraj na wanamgambo wa Haftar
Apr 12, 2020 12:13Mapigano makali yanaripotiwa kuendelea nchini Libya baina ya vikosi vya Serikali ya Maafikiano ya Kitaifa inayoongozwa na Fayez al-Sarraj na wanamgambo watiifu kwa jenerali muasi Khalifa Haftar.
-
Vikosi vya Haftar vyafanya hujuma ya kukata umeme katika mji mkuu wa Libya, Tripoli
Apr 11, 2020 04:15Vikosi vya kundi linalojiita Jeshi la Taifa la Libya (LNA) linaloongozwa na jenerali muasi Khalifa Haftar vimefanya hujuma ya kusababisha umeme kukatika katika baadhi ya maeneo ya mji mkuu wa Libya, Tripoli.
-
Vikosi vya Haftar vyadai vimetungua drone 2 za Uturuki huko Libya
Apr 09, 2020 08:21Kundi la wanamgambo wanaojiita Jeshi la Tifa la Libya wanaoongozwa na jenerali Khalifa Haftar linadai kuwa limetungua ndege mbili zisizo na rubani za Uturuki zilizokuwa zikiruka katika anga ya nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
-
UN yalaani shambulio la wanamgambo wa Haftar dhidi ya hospitali ya wagonjwa wa Corona Libya
Apr 08, 2020 13:10Umoja wa Mataifa umelaani vikali shambulio lililofanywa na wanamgambo watiifu kwa jenerali muasi nchini Libya Khalifa Haftar dhidi ya hospitali ya kulazwa wagonjwa wa virusi vya Corona kusini mwa mji mkuu wan chi hiyo Tripoli.
-
Vikosi vya serikali ya Libya vyaripua ndege yenye shehena ya silaha ya kundi la Khalifa Haftar
Apr 06, 2020 07:44Vikosi vya Serikali ya Maafikiano ya Kitaifa ya Libya (GNA) vimeiteketeza ndege moja iliyokuwa imebeba shehena ya silaha na zana za kijeshi kwa ajili ya kundi linalojiita Jeshi la Taifa la Libya (LNA) linaloongozwa na Khalifa Haftar.
-
UN yataka kusitishwa vita haraka nchini Libya na kutiliwa maanani virusi vya corona
Apr 05, 2020 10:48Ofisi ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Libya imetoa wito wa kusitishwa mapigano mara moja na kusitishwa vita nchini humo kwa ajili ya kukabiliana na maambukizi ya virusi vya corona.