-
Iran: Marekani haina azma ya kufunga jela ya Guantanamo
Jan 13, 2022 23:23Mkuu wa Masuala ya Kimataifa wa Idara ya Mahakama ya Iran ameukosoa vikali utawala wa Rais Joe Biden wa Marekani kwa kufeli kutekeleza ahadi yake ya kufunga jela ya kutisha ya Guantanamo Bay iliyoko nchini Cuba.
-
Brigedia Jenerali Shekarchi: Marekani ni mfadhili mkuu wa ugaidi, chanzo cha ukosefu wa usalama duniani kote
Jan 11, 2022 10:46Msemaji wa Jeshi la Iran ameitaja Marekani kuwa nchi inayoongoza kwa kufadhili ugaidi duniani na kusema Washington ndiyo chanzo cha ukosefu wa usalama kote duniani.
-
Uchunguzi: Wabunge 1,700 wa Kongresi ya US wamewahi kumiliki watumwa
Jan 11, 2022 04:22Uchunguzi mpya umefichua kuwa, zaidi ya watu 1,700 waliowahi kuhudumu katika Kongresi ya Marekani wamewahi kuwamiliki wanadamu kama bidhaa, hali inayoonesha biashara ya utumwa ilivyokuwa imekita mizizi nchini humo.
-
Waliohukumiwa kifo Marekani wafadhilisha 'risasi' badala ya sindano ya sumu
Jan 11, 2022 04:20Wafungwa wawili waliohukumiwa kifo katika jimbo la Oklahoma nchini Marekani wameenda mahakamani kutaka kuangaliwa upya namna ya utekelezaji wa hukumu ya kifo nchini humo.
-
Wataalamu wa UN waitaka Marekani ifunge gereza la Guantamano
Jan 11, 2022 04:19Wataalamu wa Umoja wa Mataifa wameutaka utawala wa Rais Joe Biden wa Marekani utekeleze ahadi yake ya kufunga jela ya kutisha ya Guantanamo Bay iliyoko nchini Cuba.
-
Wanajeshi magaidi wa Marekani waiba makumi ya malori ya mafuta ya Syria
Jan 10, 2022 08:33Duru za kiusalama za Syria zimetangaza kuwa, muungano vamizi unaoongozwa na wanajeshi magaidi wa Marekani umeiba malori mengine 79 ya mafuta ya Syria na kuyaingiza nchini Iraq.
-
Iran yaikosoa Marekani kwa kuingiza udikteta kwenye michezo
Jan 09, 2022 23:19Rais wa Kamati ya Taifa ya Olimpiki ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeikashifu na kuikosoa vikali Marekani kwa hatua yake ya kususia Michezo ya Olimpiki ya Msimu wa Baridi Kali itakayofanyika huko Beijing, China.
-
Instagram yafuta jumbe zinazozungumzia Jenerali Soleimani
Jan 08, 2022 09:02Wananchi wa Iran wameanzisha kampeni ya kulalamikia hatua ya mtandao wa kijamii wa Instagram ya kuendelea kufuta jumbe zinazohusiana na Luteni Jenerali Qasem Soleimani, aliyekuwa Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Sisitizo la China la kuitaka Marekani iiondolee vikwazo Iran
Jan 07, 2022 04:02Kabla ya kuanza duru ya nane ya mazungumzo ya Vienna kuhusu JCPOA, China imeitaja Marekani kuwa mhusika katika uvurugaji mapatano ya JCPOA na hivyo imeitaka isitishe utekelezaji wa sera zake za vikwazo na mashinikizo ya juu zaidi dhidi ya Iran. Zhao Lijian Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China amesema ni wazi kuwa, kwa mtazamo wa kisheria na kimaadili, vikwazo vyote vya Marekani dhidi ya Iran vinapaswa kuondolewa.
-
Zaidi ya Watu laki saba wengine wagunduliwa kukumbwa na corona siku moja nchini Marekani
Jan 06, 2022 09:04Data mpya zilizotolewa na serikali ya Marekani kuhusu wagonjwa wa UVIKO-19 au corona nchini humo zinaonesha kuwa, nchi hiyo ya Magharibi inaendelea kuvunja rekodi za mataifa mengine duniani kwa idadi kubwa ya wagonjwa wa corona. Zaidi ya watu laki saba wengine wamepatikana wana ugonjwa huo nchni humo katika kipindi cha siku moja.