-
Visingizio vinavyotumiwa na Marekani kuzuia misaada kwa nchi maskini duniani
Jun 12, 2021 22:50Wakati maambukizi ya virusi vya corona na ugonjwa wa COVID-19 vikiendelea kusababisha mgogoro wa kiuchumi na umaskini katika nchi mbalimbali duniani na kuzifanya nchi hizo zihitajie misaada zaidi ya nchi tajiri, maafisa wa serikali ya Marekani wanafanya mikakati ya kuzuia misaada kwa nchi hizo kwa kutumia visingizio vya aina mbalimbali.
-
Waandishi habari wa Marekani wataka kuakisiwa jinai za Israel katika vyombo vya habari vya nchi hiyo
Jun 12, 2021 22:20Zaidi ya Waandishi wa habari 500 wa Marekani wamesaini barua ya pamoja wakitaka kuakisiwa na kutangazwa habari zinazohusiana na dhulma na siasa za kibaguzi za Israel huko Palestina.
-
Iran: Marekani inalia machozi ya mamba, haijaachana na sera za Trump
Jun 12, 2021 08:36Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Anayehusika na Masuala ya Kisiasa amesema ni kinaya kuiona Marekani inalia machozi ya mamba katika hali ambayo Washington inaendeleza jitihada zake za kuwataabisha na kuwahangaisha kwa njaa na umaskini Wairani milioni 82.
-
Mangoush: Libya haitaruhusu ardhi yake itumiwe dhidi ya nchi nyingine
Jun 11, 2021 22:21Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa nchini Libya amesema kuwa nchi yake haitakubali kutumiwa kama kituo cha kuvuruga amani na utulivu katika kanda hiyo ya Afrika au kutumiwa ardhi na anga yake dhidi ya upande wowote mwingine.
-
Hatua mpya za vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran
Jun 11, 2021 08:25Wizara ya Biashara ya Marekani Alkhamisi ya jana iliwaweka watu na mashirika kadhaa katika orodha yake ya vikwazo kwa kisingizio cha nafasi yao katika kudhamini fedha kwa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (Sepah) na harakati ya wapiganaji wa kujitolea ya Ansarullah nchini Yemen.
-
Russia yaanza mazoezi ya kijeshi eneo ambako Marekani pia inapanga mazoezi ya kivita
Jun 11, 2021 07:53Jeshi la Majini la Russia limeanza mazoezi makubwa ya kijeshi katika eneo la kati mwa Bahari ya Pasifiki punde baada ya Marekani kusema itafanya mazoezi makubwa zaidi ya kivita katika eneo hilo hilo katika msimu wa joto mwaka huu.
-
Ansarullah: Marekani inafadhilisha vita Yemen, haitaki amani
Jun 11, 2021 03:25Mwenyekiti wa Kamati Kuu ya Mapinduzi ya Yemen amelaani hatua ya Marekani ya kuliwekea vikwazo vipya taifa hilo la Kiarabu na kusisitiza kuwa, Washington inafadhilisha vita nchini Yemen, na wala haitaki amani kama inavyodai.
-
Pentagon yaingiwa na kiwewe baada ya manowari za Iran kuwasili Atlantic
Jun 10, 2021 22:22Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) imeingiwa na kiwewe na wahaka mkubwa baada ya msafara wa meli za kijeshi za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuwasili katika Bahari ya Atlantic pasi na kupitia katika bandari za nchi nyingine kwa mara ya kwanza katika historia.
-
Russia: Wanajeshi wa Marekani nchini Syria ni wavamizi, waondoke
Jun 09, 2021 07:08Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema kuwa, wanajeshi wa Marekani ni wavamizi nchini Syria na wako huko kinyume cha sheria, hivyo wanapaswa waondoke.
-
Eritrea yailaumu Marekani kwa kuchochea mapigano Tigray, Ethiopia
Jun 08, 2021 03:42Waziri wa Mambo ya Nje wa Eritrea amezilaumu tawala za Marekani kwa kuchochea mapigano na vita katika eneo la Tigray, la kaskazini mwa Ethiopia kwa zaidi ya miongo miwili sasa.