-
HAMAS: Mpango wa Israel wa kupora ardhi za Ukingo wa Magharibi utagonga mwamba
Sep 24, 2020 08:29Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema kuwa, njama za Marekani na utawala haramu wa Israel za kutaka kutwaa ardhi zaidi katika Ukingo wa Magharibi na kuziunganisha na ardhi nyingine zilizoghusubiwa za Palestina zitashindwa na kugonga ukuta.
-
Mivutano baina ya Marekani na China yashadidi baada ya hotuba ya Trump katika Umoja wa Mataifa
Sep 24, 2020 04:40Katika hotuba yake ya mwisho kwenye ukumbi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa katika kipindi chake cha kwanza cha urais wa Marekani, Donald Trump amejikita zaidi katika masuala ya China na Iran na kudai kuwa, Marekani imejiondoa katika makubaliano mabaya sana ya nyuklia ya JCPOA na imeiwekea Iran vikwazo vya kulema.
-
Venezuela yaunda kikosi maalumu cha makomando kukabiliana na chokochoko za Marekani
Sep 23, 2020 23:12Rais Nicolas Maduro wa Venezuela ameukosoa vikali ujambazi na umafia unaofanywa na serikali ya Marekani dhidi ya nchi yake na ametangaza habari ya kuundwa kikosi maalumu cha makomando cha kupambana na vitendo vya kiharibifu vya Marekani.
-
Rouhani: tuhuma na mahesabu ghalati ya Saddam zinakaririwa leo na Marekani
Sep 23, 2020 09:56Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria vita vya kiuchumi vya Marekani dhidi ya Iran na kusema: tuhuma na mahesabu ghalati ya viongozi wa White House yanafanana na hatua zilizochukuliwa na utawala wa Saddam na kupelekea kuangamizwa utawala huo.
-
Balozi wa Iran UN: Vikwazo vya Marekani ni jinai dhidi ya binadamu
Sep 23, 2020 03:49Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Ofisi ya Umoja wa Mataifa iliyoko mjini Geneva Uswisi amesema vikwazo vya upande mmoja vya Marekani dhidi ya Iran ni jinai dhidi ya binadamu.
-
Russia kuendelea kushirikiana kijeshi na Iran licha ya vikwazo vya Marekani
Sep 22, 2020 22:04Seneta mmoja wa Russia amesema nchi hiyo itaendelea kuwa na ushirikiano na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika uga wa kijeshi licha ya uhasama, vikwazo na mashinikizo ya Marekani.
-
Kushadidi upinzani dhidi ya safari ya Mike Pompeo katika eneo la Amerika ya Latini
Sep 22, 2020 06:57Safari ya Mike Pompeo, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani katika nchi nne za Amerika ya Latini, licha ya kuwa imefanyika kwa ajili ya kuongeza mbinyo na mashinikizo dhidi ya Venezuela, lakini imekabiliwa na malalamiko na upinzani wa makundi mengi ya wanaharakati wa amani na vyama mbalimbali katika mataifa hayo.
-
Pelosi: Uzembe wa serikali ya Trump katika kupambana na corona umesababisha vifo vya maelfu ya watu
Sep 22, 2020 04:55Spika wa Kongresi ya Marekani kwa mara nyingine tena amekosoa utendaji wa serikali ya Rais Donald Trump wa nchi hiyo katika kupambana na virusi vya corona.
-
Kiongozi wa Ansarullah: Mapinduzi ya Septemba 21 ya wananchi wa Yemen yalikuwa mwanzo wa kuondokana na giza la huko nyuma
Sep 22, 2020 04:13Kiongozi wa harakati ya Ansarullah ya Yemen amesema kuwa mapinduzi ya tarehe 21 Septemba nchini humo yalikuwa mwanzo wa kupatikana njia ya kujiondoa katika giza la huko nyuma na hatua ya kujenga mustakbali kwa mujibu wa thamani na misingi ya watu wa Yemen.
-
Msimamo mmoja wa kundi la 4+1 mbele ya madai hewa ya Marekani kuhusu Iran
Sep 21, 2020 07:03Licha ya Marekani kutoa madai hewa ya kuanza kutekelezwa vikwazo vya kimataifa dhidi ya Iran kuanzia jana Jumapili Septemba 20, 2020 vikiwemo vikwazo vya silaha, lakini mataifa ya dunia yamepinga madai hayo ya Washington na yamechukua msimamo imara kiasi kwamba inaonekana kama vile hakuna mabadiliko yoyote yaliyotokea.