Wasiwasi wa kuibuka ghasia huku siku ya uchaguzi ikikaribia Marekani
https://parstoday.ir/sw/news/world-i64370-wasiwasi_wa_kuibuka_ghasia_huku_siku_ya_uchaguzi_ikikaribia_marekani
Kuna wasiwasi mkubwa kuwa kutaibuka machafuko na ghasia nchini Marekani baada ya upigaji kura siku ya Jumanne.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Nov 01, 2020 08:26 UTC
  • Wasiwasi wa kuibuka ghasia huku siku ya uchaguzi ikikaribia Marekani

Kuna wasiwasi mkubwa kuwa kutaibuka machafuko na ghasia nchini Marekani baada ya upigaji kura siku ya Jumanne.

 Olivia Katbi Smith, mkurugenzi mwenza wa Taasisi ya Democratic Socialists amenukuliwa na gazeti la Washington Post akisema, mrengo wa kulia wa Warepublican hauko tayari kuachia ngazi na hivyo kuna uwezekano wa kuibuka ghasia. Amesema watu wenye misimamo mikali katika kambi mbili hasimu za kisiasa wanaweza kukabiliana mjini Portland jimboni Oregon, mji ambao umekuwa medani ya ghasia na nembo ya mgawanyiko wa kisiasa Marekani.

Rais Donald Trump wa Marekani amekuwa akihimiza chuki katika mikutano yake ya kisiasa huku ununuzi wa bunduki ukivunja rekodi nchini humo.

Rais Trump wa Marekani

Hivi sasa katika mitandao ya kijamii ya Marekani kuna tetesi kuwa yamkini vita vya wenywe kwa wenyewe vikaibuka nchini humo iwapo ghasia zitaibuka na kuchukua mkondo tafauti baada ya uchaguzi wa Novemba tatu.

Katika siku za hivi karibuni kumeshuhudiwa makabiliano baina ya wanagambo wa mrengo wa kulia na wanaharakati wa kijamii kote Marekani hasa wakati wa maandamano ya kupinga ukatili wa polisi na ubaguzi wa rangi.

Huku uchaguzi nchini humo utakaofanyika Jumanne ukikaribia, uchunguzi wa  maoni uliochapishwa na Washington Post unaonyesha kuwa mgombea wa chama kikuu cha upinzani cha Democrat, Joe Biden anaongoza kitaifa kwa zaidi ya pointi tisa.