-
Ngao ya makombora ya Syria yazima mashambulizi ya anga ya Israel
Sep 01, 2020 03:14Jeshi la Syria limetangaza kuwa, mfumo wake wa ulinzi wa anga umefanikiwa kutungua makombora ya utawala wa Kizayuni wa Israel kusini mwa mji mkuu wa nchi hiyo ya Kiarabu, Damascus.
-
Congress: Trump ndiye sababu ya kuongezeka machafuko nchini Marekani
Aug 31, 2020 22:02Mkuu wa Kamati ya Kutoa Taarifa ya Baraza la Congress la Marekani amemlaumu vikali rais wa nchi hiyo Donald Trump na kusema kuwa, vitendo vya kichochezi vya rais huyo ndiyo sababu ya kuzuka na kuongezeka machafuko nchini Marekani.
-
Iran: Magaidi wa MKO wanapewa hifadhi na US na EU licha ya kuua maelfu ya Wairani
Aug 30, 2020 06:32Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imesema nchi za Ulaya na Marekani zinawapa hifadhi wanachama wa kundi la kigaidi la Munafikin (MKO) licha ya genge hilo kuua kikatili maelfu ya Wairani.
-
Maandamano ya 'Risasi 7, Siku 7' yafanyika Kenosha, Marekani kumlilia raia mweusi Jacob Blake
Aug 30, 2020 03:46Zaidi ya Wamarekani elfu moja wameandamana katika mji wa Kenosha kulalamikia ukatili unaofanywa na polisi wa Marekani, ikiwa imepita takribani wiki moja tangu askari mmoja alipompiga risasi saba mgongoni Jacob Blake kijana Mmarekani mweusi mwenye umri wa miaka 29 na kumfanya apooze kuanzia kiunoni hadi miguuni.
-
China yaonya: Ikilazimu, tutaingia katika makabiliano ya kijeshi na Marekani
Aug 29, 2020 19:31Jeshi la China limetahadharisha kuwa, huenda litalazimika kuingia katika makabiliano ya kijeshi na Marekani pasi na kukusudia iwapo Washington haitasitisha operesheni zake za kichokozi katika Bahari ya Kusini ya China.
-
Umbumbumbu wa Marekani katika masuala ya sheria, wameshindwa na sasa wanatoa vitisho
Aug 29, 2020 05:48Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Iran amekosoa jitihada zinazofanywa na Marekani kwa ajili ya kurejesha vikwazo vya kimataifa dhidi ya Iran kuanzia tarehe 20 Oktoba mwaka huu wa 2020 na kusema: Viongozi wa serikali ya Marekani ni mbumbumbu katika masuala ya sheria na hawajui lolote kuhusiana na tendaji wa Umoja wa Mataifa.
-
Zarif aipa Marekani somo la sheria baaada ya kubwagwa mara 3 katika UNSC
Aug 29, 2020 03:09Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameeleza kushangazwa kwake na kitendo cha Marekani cha kutishia tena kumwekea vikwazo mtu au taasisi yoyote inayoshirikiana na Iran, licha ya kupigwa mweleka mara tatu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Askari wa Saudia waingia katika kambi ya kijeshi ya Marekani nchini Syria
Aug 29, 2020 02:02Saudi Arabia imetuma makumi ya wanajeshi wake katika kambi ya kijeshi ya Marekani katika mkoa wenye utajiri wa mafuta wa Hasakah, huko kaskazini mashariki mwa Syria. Hayo yameripotiwa na kanali ya televisheni ya al-Mayadeen ya Lebanon.
-
Iran: 'Mashariki ya Kati' mpya itaanzishwa kwa kutimuliwa Marekani katika eneo
Aug 28, 2020 08:05Msaidizi maalumu wa Spika wa Bunge la Iran katika masuala ya kimataifa amesema: 'Mashariki ya Kati' mpya itaundwa baada ya kuhakikisha Marekani imeshatimuliwa kikamilifu katika eneo hili la Asia Magharibi.
-
Msimamo wa kukinzana wa Marekani kuhusu mgogoro wa nyuklia wa Korea
Aug 28, 2020 05:42Takriban ni miongo 7 sasa ambapo Marekani ina wanajeshi wake katika Rasi ya Korea. Licha ya kufanyika mazungumzo mara kadhaa baina ya viongozi wa Marekani na Korea Kaskazini kuhusu kupokonywa silaha za nyuklia Pyongyang lakini mgogoro wa Korea mbili bado uko vile vile. Si hayo tu lakini rais wa Marekani, Donald Trump hivi sasa anataka kupunguzwa idadi ya wanajeshi wa nchi hiyo huko Korea Kusini, suala ambalo limezusha mzozo mpya.