-
Malalamiko ya Ujerumani kwa vitisho vya Marekani dhidi ya usalama wa nishati barani Ulaya
Jun 15, 2020 03:30Baada ya Donald Trump kuingia katika Ikulu ya Marekani, White House, uhusiano wa Washington na Umoja wa Ulaya ikiwemo Ujerumani umevurugika na kufikia kiwango cha chini kabisa. Uhusiano huo umezidi kuwa mbaya baada ya Trump kuzungumzia suala la kuondoa wanajeshi wa Marekani huko Ujerumani.
-
Kuungana watu wa Ulaya na maandamano ya kupinga ubaguzi wa rangi nchini Marekani
Jun 14, 2020 21:53Ukandamizaji na utumiaji mabavu wa polisi ya Marekani dhidi ya Wamarekani wenye asili ya Afrika licha ya kuwa una historia kongwe, lakini kuuawa Mmarekani mweusi George Floyd jinai iliyofanywa na polisi mweupe katika mji wa Minneapolis kwenye jimbo la Minnesota, sio tu kwamba, kumewasha moto wa malalamiko na maandamano ambayo hayajawahi kushuhudiwa katika miji mbalimbali ya Marekani, bali malalamiko hayo yameenea hadi katika nchi za bara Ulaya.
-
Mazungumzo kuhusu ubaguzi wa kizazi; mwito wa nchi za Afrika kwa Baraza la Haki za Binadamu
Jun 13, 2020 23:14Kuuliwa kikatili Mmarekani Mwafrika, Geroge Floyd, kulikofanywa na polisi mzungu tarehe 25 Mei huko Minneapolis, katika jimbo la Minnesota nchini Marekani si tu kumezusha wimbi kubwa la maandamano ndani ya nchi hiyo, bali dunia nzima imeripuka kwa maandamano ya kushinikiza mapambano ya kweli dhidi ya ubaguzi wa rangi na ukatili wa jeshi la polisi la Marekani.
-
UN yataka kufanyika marekebisho ya haraka katika muundo wa polisi Marekani
Jun 13, 2020 00:09Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Kutokomeza Ubaguzi wa Rangi jana Ijumaa iliitaka serikali ya Marekani kutetekeleza marekebisho haraka iwezekanavyo kwa ajili ya kuondoa ubaguzi wa rangi wa kimfumo katika muundo wa polisi ya nchi hiyo.
-
China yapinga kurefushwa vikwazo vya silaha dhidi ya Iran
Jun 12, 2020 23:41Kwa mara nyingine tena China imepinga vikali njama za Marekani za kutaka kurefushwa muda wa vikwazo vya silaha dhidi ya Iran. Muda wa vikwazo hivyo unafikia tamati Oktoba mwaka huu wa 2020, kwa mujibu wa Azimio Nambari 2231 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Joe Biden: Trump atafanya jaribio la kuiba kura za uchaguzi wa rais, atang’ang’ania White House
Jun 12, 2020 06:45Mgombea kiti cha rais wa Marekani kwa tiketi ya chama cha Democratic, Joe Biden amesema kuwa ana wasiwasi kwamba Rais Donald Trump wa nchi hiyo atafanya jaribio la kuiba kura iwapo atashindwa katika uchaguzi ujao wa rais.
-
Matokeo mabaya ya vitendo viovu vya Marekani dhidi ya Iran; kuendelea kuvunjwa sheria duniani
Jun 12, 2020 05:47Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, Marekani haina haki ya kuutumia vibaya Umoja wa Mataifa na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA kuiharibia jina Iran.
-
Katibu Mkuu wa NATO akiri: Mlingano wa nguvu duniani umebadilika
Jun 12, 2020 03:32Marekani ambayo ni kinara wa nchi za Magharibi imekuwa ikipinga suala la kuongezeka nguvu, ustawi na satua ya China katika uwanja wa kimataifa na imeitambua nchi hiyo kuwa ni tishio kwa ulimwengu wa Magharibi ikizitaka nchi za Ulaya kupunguza uhusiano wao na Beijing.
-
Masanamu yanayoashiria ubaguzi yaendelea kuvunjwa Marekani na waandamanaji wenye hasira
Jun 12, 2020 03:23Waandamanaji wenye hasira nchini Marekani na maeneo mengine duniani wanaendeleza mkakati wa kuangusha, kuharibu na kuondoa masanamu ya wabaguzi wa rangi.
-
Mapatano ya Washington na Baghdad kuhusu kupunguzwa askari wa Marekani nchini Iraq
Jun 12, 2020 03:16Kumefikiwa mapatano ya kupunguzwa askari wa Marekani nchini Iraq. Mapatano hayo yamefikiwa Alhamisi katika mkutano uliofanyika baina ya Abdulkarim Hashemi Mustafa mwakilishi wa serikali ya Iraq na David Hale mwakilishi wa serikali ya Marekani.