-
TV na redio za fitna za Saudia na Marekani zapigwa marufuku Iraq
Oct 27, 2019 23:05Serikali ya Iraq imezipiga marufuku televisheni tatu na redio moja za Marekani na Saudi Arabia kwa kueneza fitna na machafuko nchini Iraq.
-
Abubakr al-Baghdadi, kiongozi wa Daesh auawa
Oct 27, 2019 04:08Afisa mmoja wa Pentagon nchini Marekani amesema kuwa Abubakr al-Baghdadi, kiongozi wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh ameuawa katika operesheni ya siri iliyotekelezwa kaskazini magharibi mwa Syria.
-
Picha za satalaiti zathibitisha; Marekani inafanya magendo ya mafuta ya Syria
Oct 26, 2019 08:53Russia imesema picha za satalaiti zimetoa ithibati kuwa Marekani inafanya magendo ya mafuta ya Syria chini ya ulinzi wa vikosi vyake vya usalama.
-
Nakisi ya bajeti ya Marekani yakaribia dola trilioni moja
Oct 26, 2019 08:32Serikali ya Marekani imemaliza mwaka huu wa kifedha wa 2019 kwa nakisi ya bajeti inayokaribia dola trilioni moja, ikiwa ni kiwango kikubwa zaidi cha nakisi kuwahi kushuhudiwa nchini humo ndani ya miaka saba iliyopita.
-
Raia 3 wa Somalia 'watoweka' kufuatia shambulizi la anga la Marekani
Oct 26, 2019 08:27Kwa akali raia watatu wanahofiwa kuuawa katika shambulizi la anga lililofanywa na ndege isiyo na rubani 'drone' ya Marekani katika eneo la Puntland, kaskazini mashariki mwa Somalia.
-
Mwanafunzi wa Kiislamu Marekani aondolewa mashindanoni kwa kuvaa hijabu
Oct 26, 2019 08:24Mwanafunzi wa kike wa shule moja katika jimbo la Ohio nchini Marekani ameondolewa kwenye mashindano ya mbio za nyika kwa kuvaa vazi la stara la hijabu.
-
Trump aendelea kutoa misimamo ya nyuso mbili kuhusu Wakurdi wa Syria
Oct 25, 2019 03:40Rais wa Marekani kwa mara nyingine tena ametia ulimi puani na kubadilisha msimamo wake wa huko nyuma kuhusu Wakurdi wa Syria. Katika ujumbe wake mpya wa Twitter sasa Trump amewataka Wakurdi hao waende wakajikusanye kwenye maeneo yenye utajiri wa mafuta.
-
Safari ya Waziri wa Ulinzi wa Marekani nchini Saudia na madai ya kuulinda utawala wa Aal Saud
Oct 23, 2019 12:37Rais Donald Trump wa Marekani daima amekuwa akidai kuwa, anawahami na kuwalinda waitifaki wake wa Mashariki ya Kati, na katika uwanja huo Saudi Arabia ambayo ni mshirika mkuu wa Washington ina nafasi maalumu katika siasa za kikanda za White House.
-
Takwimu: Watu wanaojiua wazidi kuongezeka nchini Marekani
Oct 23, 2019 09:44Vyombo vya habari nchini Marekani vinaripoti kuwa, vitendo vya kujiua vimeongezeka mno nchini humo hususan baina ya vijana.
-
Makeke ya Trump mbele ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
Oct 22, 2019 08:20Donald Trump Rais wa Marekani mwenye kubwabwaja sana tangu aingie ikulu ya White House amechukua mkondo wa sera za chuki na uhasama dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na utendaji wake umejikita katika mashinikizo ya kiwango cha juu kabisa dhidi ya Tehran ili kwa njia hiyo aweze kulifanya taifa hili lisalimu amri na kukubali matakwa ya Washington.