-
Zarif amwambia Trump, kaulimbiu ya Netanyahu ni: Tutapigana vita hadi askari wa mwisho wa Marekani
Sep 10, 2019 22:54Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amemtumia ujumbe wa Twitter Rais Donald Trump wa Marekani akisema: Kaulimbiu ya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu ni: Tutapigana vita hadi atakapobakia askari wa mwisho kabisa wa Marekani.
-
Nasrullah: Hizbullah na Iran haziwezi kuyumbishwa na mashinikizo
Sep 10, 2019 02:47Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema harakati hiyo ya muqawama na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran zitaendelea kusimama kidete dhidi ya mashinikizo na vikwazo vya Marekani.
-
Mwakilishi wa Iran UN: Marekani imekiuka mkataba wa NPT
Sep 09, 2019 22:08Mwakilishi wa kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa ametilia mkazo jukumu la pamoja la kupiga marufuku aina yoyote ya majaribio ya uripuaji silaha za nyuklia na kueleza kwamba Marekani imekiuka mkataba wa kuzuia uundaji na uenezaji silaha za nyuklia (NPT) kwa kujitoa kwenye makubaliano yanayohusiana na mkataba huo na kwa kuanzisha mashindano ya kuzifanya silaha hizo za nyuklia kuwa za kisasa zaidi.
-
Trump afutilia mbali kikao cha siri na Taliban
Sep 09, 2019 01:33Katika kipindi cha kampeni za uchaguzi wa rais wa Marekani, Rais Donald Trump wa nchi hiyo aliahidi kuwaondoa askari wote wa Marekani wanaohudumu Afghanistan.
-
Syria yalaani doria ya Marekani na Uturuki katika ardhi yake, yasema ni uvamizi
Sep 08, 2019 20:02Serikali ya Syria imelaani hatua ya majeshi ya Marekani na Uturuki ya kupiga doria ya pamoja katika eneo liliilopewa jina la "ukanda wa amani" huko mashariki mwa Furati kaskazini mwa Syria na kusema ni ukiukaji wa sheria za kimataifa na mamlaka ya kujitawa ya Syriia.
-
Sisitizo la Corbyn la kukabiliana na muungano wa Netanyahu na Trump dhidi ya JCPOA
Sep 07, 2019 01:50Tangu yalipofikiwa makubaliano ya nyuklia ya Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA) mwaka 2015, Marekani na utawala wa Kizayuni zimekuwa zikisisitiza kila mara kuwa zinayapinga makubaliano hayo na kutaka yavunjwe. Na katika hatua iliyolenga kufikia lengo hilo, mwezi Mei 2018, Rais Donald Trump wa Marekani alitangza kujitoa nchi yake kwenye makubaliano hayo na kuanza kutekeleza vikwazo vikali ambavyo havijawahi kushuhudiwa dhidi ya Iran.
-
Hatua mpya za Marekani dhidi ya JCPOA; kupinga mpango wa Ufaransa na kutangaza vikwazo vipya dhidi ya Iran
Sep 05, 2019 21:55Rais Donald Trump wa Marekani alisikika mara kadha wa kadha akiyakosoa vikali makubaliano ya nyuklia ya JCPOA, na hatimaye mnamo tarehe 8 Mei, 2018 akatangaza rasmi kujitoa nchi yake katika makubaliano hayo. Kilichofuata baada ya hapo, ilikuwa ni kutekelezwa na serikali ya Trump katika awamu mbili tofauti vikwazo vikali dhidi ya Iran sambamba na kupinga mpango wowote wa kuyalinda makubaliano hayo ya nyuklia.
-
Mousavi: Matamshi ya uhasama hayafiki popote
Sep 05, 2019 02:51Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa matamshi ya uhasama ya Brian Hook Mjumbe Maalumu wa Marekani katika masuala ya Iran hayatafika popote.
-
Juhudi mpya za Kongresi za kutaka kuzuia himaya ya Trump kwa Saudia na washirika wake, Yemen
Sep 04, 2019 00:00Marekani imekuwa na nafasi kubwa sana katika vita na mauaji yanayoendelea kufanywa na Saudi Arabia na washirika wake huko Yemen kutokana na misaada ya himaya yake ya kilojistiki, kipelelezi na zana za kivita kwa muungano huo. Suala hilo sambamba na ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu unaofanywa na utawala wa kifalme wa Saudia, vimezidisha malalamiko na upinzani dhidi ya misaada na ushirikiano wa kijeshi wa Marekani na Saudia na washiriki wake katika vita vya Yemen.
-
Kushadidi makabiliano baina ya Boris Johnson na wapinzani wake kuhusiana na Brexit
Sep 03, 2019 22:08Kujitoa Uingereza katika Umoja wa Ulaya (Brexit) limegeuka na kuwa suala muhimu hivi sasa katika siasa za ndani na za nje za London.