-
Ansarullah: Marekani na Uingereza zijiandae 'kulipa gharama kubwa' kwa kuishambulia Yemen
Jan 12, 2024 04:14Harakati ya Muqawama ya Ansarullah ya Yemen imezilaani vikali Marekani na Uingereza baada ya kufanya mashambulizi makali dhidi ya vituo vyake ndani ya Yemen, na kuonya kuwa vituo vya kijeshi vya nchi hizo vilivyoko katika eneo vitashambuliwa iwapo zitafanya uchokozi zaidi.
-
Marekani inanunua mafuta kutoka Russia licha ya kujiwekea marufuku ya uagizaji
Jan 12, 2024 03:31Marekani imeendelea kununua mafuta ya Russia licha ya kuwa mtetezi mkuu wa vikwazo dhidi ya nchi hiyo na kujiwekea marufuku tokea mwanzoni mwa mwaka 2022 ya kuagiza nishati kutoka nchini humo.
-
Jeshi la Wanamaji la Iran lakamata meli ya mafuta ya Marekani kwa amri ya mahakama
Jan 11, 2024 12:06Jeshi la Wanamaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limetangaza kuikamata meli ya mafuta ya Marekani kwa amri ya mahakama katika Bahari ya Oman.
-
Al Sudani asisitiza kuondoka haraka wanajeshi vamizi wa Marekani huko Iraq
Jan 11, 2024 04:16Waziri Mkuu wa Iraq ameashiria hatua za kuvuruga usalama na amani vya Marekani na kutaka kuondoka nchini humo wanajeshi vamizi wa Marekani haraka iwezekanavyo.
-
Njama za Marekani za kuendelea kubakia kijeshi nchini Iraq
Jan 11, 2024 03:44Licha ya serikali ya Iraq kuitaka Marekani iondoe wanajeshi wake nchini humo, lakini Washington imetangaza kuwa, haina ratiba yoyote ya kutoka katika nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Iran na Russia: Marekani inatafuta visingizio vya kupanua uwepo wake katika eneo
Jan 10, 2024 03:22Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Hossein Amir-Abdollahian na mwenzake wa Russia Sergei Lavrov wamesema Marekani inajaribu kubuni visingizio ili kupanua uwepo wake katika eneo. Wanadiplomasia hao wakuu wa Tehran na Moscow wametoa indhari hiyo katika mazungumzo waliyofanya kwa njia ya simu jana Jumanne.
-
Kufichuliwa nafasi ya jasusi wa Uholanzi katika hujumu dhidi ya vituo vya nyuklia vya Iran
Jan 10, 2024 02:34Gazeti la Volkskrant la Uholanzi limefichua kuwa, raia mmoja wa nchi hiyo alikuwa na mchango mkubwa katika operesheni ya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel ya kuhujumu kituo cha kurutubisha uranium cha Natanz nchini Iran.
-
Ombi la Italia la kuunda jeshi la Ulaya
Jan 08, 2024 22:45Waziri wa Mambo ya Nje wa Italia, Antonio Tajani, amesema kwamba Umoja wa Ulaya unapaswa kuunda jeshi lake la pamoja ambalo linaweza kuwa na jukumu la kudumisha amani na kuzuia migogoro.
-
China yayawekea vikwazo makampuni matano ya Marekani kwa kuiuzia silaha Taiwan
Jan 08, 2024 03:09Wizara ya Mambo ya Nje ya China imetangaza vikwazo dhidi ya makampuni matano ya Marekani kwa kuiuzia Taiwan silaha.
-
Maafisa wa Intelijensia wa Marekani: Israel haitaweza kushinda vita dhidi ya Hizbullah
Jan 08, 2024 02:47Gazeti la Washington Post limeripoti kuwa, tathmini ya siri iliyofanywa na Shirika la Ulinzi wa Intelijensia la Marekani (DIA) imegundua kwamba "itaviwiya vigumu kufanikiwa" vikosi vya jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel katika vita vya medani mbili dhidi ya Hamas huko Gaza na Hizbullah huko Lebanon.