-
Al Azhar: Itungwe sheria ya kutambua hujuma dhidi ya Uislamu kuwa ni uhalifu
Oct 29, 2020 02:55Sheikh Mkuu wa al Azhar nchini Misri amekosoa matamshi ya chuki na hujuma ya Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa dhidi ya Uislamu na kutoa wito wa kutungwa sheria inayotambua chuki na uhasama dhidi ya Waislamu kuwa ni uhalifu.
-
Baada ya vitisho vya Trump IGAD yataka mazungumzo ya Ethiopia na Misri kuhusu bwawa
Oct 26, 2020 07:18Shirika la Maendeleo la Kiserikali la Nchi za Mashariki mwa Afrika (IGAD) limehimiza mazungumzo yafanyike na mwafaka ufikiwe ili kuleta suluhu kuhusu kadhia ya bwawa kubwa linalojengwa na Ethiopia kwenye Mto Nile linalojulikana kama Grand Renaissance Dam (GERD).
-
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Ethiopia: Matamshi ya Trump kuhusu bwawa la Renaissance ni ya kihalifu
Oct 25, 2020 12:10Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Ethiopia ameyataja matamshi yaliyotolewa na Rais Donald Trump wa Marekani kuhusu bwawa la Renaissance kuwa ni jinai na uhalifu.
-
Ethiopia yamwita kumsaili balozi wa Marekani kwa matamshi aliyotoa Trump
Oct 24, 2020 14:41Balozi wa Marekani mjini Addis Ababa ameitwa kusailiwa kufuatia kauli aliyotoa Rais Donald Trump wa Marekani kuhusu bwawa la An-Nahdhah au Renaissance.
-
Maelfu ya Wamisri wakamatwa katika maandamano dhidi ya utawala wa Sisi
Oct 11, 2020 12:02Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limesema kwa uchache watu elfu mbili wametiwa mbaroni katika maandamano ya kupinga utawala wa Rais Abdel Fattah al-Sisi wa Misri ndani ya siku 20 zilizopita.
-
Misri yataka vita dhidi ya magaidi nchini Syria viongezewe kasi
Oct 05, 2020 08:10Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri amefanya mazungumzo na mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa na kutilia mkazo udharura wa kupambana vilivyo na kikamilifu na magenge ya kigaidi nchini Syria.
-
Amnesty yaitaka serikali ya Misri kusitisha ukandamizaji wa wapinzani
Oct 04, 2020 02:45Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limeitaka serikali ya Misri kukomesha ukandamizaji dhidi ya wapinzani.
-
Kamanda wa jeshi la Ethiopia: Tunaweza kuzima shambulio dhidi ya al Nahdha
Oct 01, 2020 10:34Kamanda wa Jeshi la Anga la Ethiopia amekariri tena kwamba nchi yake ina uwezo wa kuziuia shambulizi lolote dhidi ya bwawa na Renaissance (al-Nahdha) linalojengwa juu ya maji ya Mto Nile ambalo limesababisha mgogoro mkubwa baina ya nchi hiyo na nchi za Misri na Sudan.
-
Wanachama 6 wa Ikhwan wahukukmiwa kunyongwa nchini Misri
Oct 01, 2020 02:28Mahakama nchini Misri imewahukumu kifo wanachama 6 wa Ikhwanul Muslimin kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya maafisa wa polisi.
-
Mamia ya raia wakamatwa Misri katika maandamano dhidi ya Rais al Sisi
Sep 29, 2020 07:29Mashirika ya kutetea haki za binadamu nchini Misri yametangaza kuwa mamia ya watu wametiwa nguvuni katika maandamano yanayofanywa na wananchi kwa siku kadhaa mtawalia wakimtaka Rais Abdel Fattah al Sisi ajiuzulu na kuondoka madarakani.