-
Watu kadhaa wauawa katika maandamano ya kumtaka Rais wa Misri ajiuzulu
Sep 26, 2020 12:21Kwa akali watu wawili wameuawa huku makumi ya wengine wakijeruhiwa katika ghasia za maandamano ya wananchi wa Misri, wanaomtaka Rais Abdel Fattah al Sisi wa nchi hiyo ang'atuke madarakani.
-
Maandamano wa wapinzani wa el Sisi yafanyika nchini Misri
Sep 19, 2020 07:27Baadhi ya wananchi wa Misri wamefanya maandamano katika mji wa Suez wa mashariki mwa mji mkuu Cairo kupinga siasa za rais wa nchi hiyo, Abdel Fattah el Sisi.
-
Mawakili: Mtoto wa Morsi aliuawa kwa kemikali ya sumu Misri
Sep 08, 2020 07:50Mawakili wa familia ya Mohammad Morsi, rais wa zamani wa Misri wamesema mtoto wa kiume wa kiongozi huyo, Abdullah Morsi aliuawa kwa kemikali hatari ya sumu, na wala hakufa kwa mshtuko wa moyo kama zilivyotangaza mamlaka za nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Human Rights Watch: Hali katika jela za Misri ni mbaya
Sep 04, 2020 11:50Shirika la kimataifa la haki za Binadamu, Human Rights Watch limetangaza habari ya kupoteza maisha wafungwa wanne katika kipindi cha chini ya masaa 72 kwenye jela za Misri na kusema kuwa hali katika jela hizo ni mbaya hasa kutokana na kudharauliwa usalama wa kiafya wa wafungwa.
-
Jeshi la Misri laangamiza magaidi zaidi ya 70 Sinai Kaskazini
Sep 01, 2020 02:32Jeshi la Misri limetangaza kuwa limeua magaidi zaidi ya 70 wenye mfungamano na genge la kigaidi la Daesh (ISIS) katika operesheni za vikosi vya usalama vya nchi hiyo katika mkoa wa Sinai Kaskazini.
-
Sudan yataka mzozo wa Bwawa la al-Nahdha ujadiliwe na marais wa nchi husika
Aug 30, 2020 11:59Serikali ya Khartoum imetoa mwito wa kujadiliwa mzozo wa Bwawa la al-Nahdha na marais wa Sudan, Misri na Ethiopia.
-
Bunge la Ugiriki laafiki mapatano ya baharini yaliyofikiwa kati ya nchi hiyo na Misri
Aug 28, 2020 07:29Bunge la Ugiriki hatimaye limepasisha mapatano yaliyofikiwa kati ya nchi hiyo na Misri ya kuianisha mipaka ya baharini.
-
Amnesty: Misri inawanyima wafungwa haki zao kwa miaka kadhaa sasa
Aug 21, 2020 00:07Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limeitaka serikali ya Misri kuziruhusu familia za wafungwa kutembea jamaa zao wanaoshikiliwa katika jela za nchi hiyo wakiwemo watetezi wa haki za binadamu na wanaharakati wa masuala ya kisiasa.
-
Ikhwanul Muslimin yalaani mapatano ya Imarati ya Israel, yasema ni usaliti dhidi ya al Aqsa
Aug 19, 2020 02:27Harakati ya Ikhwanul Muslimin ya Misri imelaani hatua ya Imarati ya kuanzisha uhusiano na utawala haramu wa Israel.
-
Mazungumzo ya viongozi wa Sudan na Misri kuhusu Bwawa la An-Nahdhah
Aug 16, 2020 07:45Waziri Mkuu wa Misri Mostafa Madbouli amefanya mazungumzo na mwenzake wa Sudan Abdalla Hamdok kuhusiana na Bwawa la An-Nahdhah au Grand Renaissance Dam (GERD) lililojengwa na Ethiopia.