-
Indhari ya Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon kwa njama za Marekani
Feb 26, 2018 07:14Sayyid Hassan Nasrullah, Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Hizbullah ya Lebanon ameashiria alipokuwa akihutubia katika mji wa Baalabek juu ya kushindwa mipango ya Marekani na washirika wake katika Mashariki ya Kati na kusambaratishwa kundi la kigaidi la Daesh na kusema kuwa, hii leo tunapaswa kukusanya mafanikio yetu ambapo kubwa zaidi katika hayo ni uungaji mkono unaopata muqawama.
-
Makundi tofauti ya Palestina yamuonya Trump juu ya kuhamishia ubalozi wa US mjini Quds
Feb 24, 2018 07:58Shakhsia na viongozi wa makundi tofauti ya Palestina yamemuonya Rais Donald Trump wa Marekani juu ya kuzidisha mgogoro wa eneo la Mashariki ya Kati kufuatia hatua yake ya kutaka kuuhamishia ubalozi wa nchi hiyo kutoka Tel Aviv kwenda mji wa Quds ambayo imepangwa kutekelezwa sawa na siku ya Nakba (inayokumbushia uvamizi wa Israel dhidi ya ardhi za Wapalestina.)
-
Kutunguliwa ndege za Magharibi walizogaiwa Saudia; mafanikio ya muqawama imara nchini Yemen
Jan 10, 2018 06:06Nguvu za kujihami za vikosi vya wananchi na jeshi la Yemen kwa mara nyingine tena zimewathibitishia wavamizi wa nchi hiyo wanaoongozwa na Saudia kwa baraka kamili za Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel kwamba Yemen sinchi inayoweza kukubali kukaliwa kwa mabavu.
-
Hizbullah: Mapambano ndio chaguo pekee la Wapalestina na Waislamu dhidi ya Marekani na Israel
Jan 01, 2018 04:21Harakati ya Mapambano ya Hizbullah ya Lebanon imetangaza kuwa, njia pekee ya Wapalestina na Waislamu kukabiliana na utawala haramu wa Israel na Marekani ni muqawama na mapambano dhidi ya tawala hizo.
-
Hizbullah: Mapambano ndio njia pekee ya Wapalestina kupata ushindi
Dec 07, 2017 14:56Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, hatua ya Rais wa Marekani ya kuutangaza mji wa Baytul Muqaddas kuwa mji mkuu wa utawala haramu wa Israel, utakuwa ni msukumo kwa watu waliokuwa kando, lakini kwa sasa wanapaswa kuingia katika medani bila ya kisingizio chochote.
-
Gebran Bassil: Jumuiya ya Nchi za Kiarabu inapaswa kutofautisha baina ya muqawama na ugaidi
Nov 25, 2017 16:10Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Lebanon ameamwandikia barua Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu (Arab League) akimwambia kwamba, umoja huo unapaswa kufungamana na makubaliano ya Waarabu ambayo yalitofautisha baina ya muqawama na ugaidi.
-
Wapalestina wakabiliana mara 290 na Wazayuni mwezi Oktoba 2017
Nov 05, 2017 03:36Wapalestina wanaoishi katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na Quds tukufu wamekabiliana mara 290 na Wazayuni katika mwezi uliopita wa Oktoba.
-
Taarifa ya mwisho ya kongamano la kimataifa la Umoja wa Wanazuoni wa Mapambano
Nov 04, 2017 02:40Kikao cha pili cha kimataifa cha Umoja wa Kimataifa wa Wanazuoni wa Mapambano kimemalizika huko Beirut mji mkuu wa Lebanon kwa kutoa taarifa inayotetea na kuunga mkono Suasla la Palestina.
-
Hizbullah ya Iraq: Baada ya Daesh kushindwa, Marekani na Israel zinapanga njama mpya
Nov 02, 2017 17:20Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu 'Kataib Hizbullah' nchini Iraq sambamba na kutangaza kuwa, genge la kigaidi na ukufurishaji la Daesh lilikuwa na mpango wa uharibifu kupitia ajenda za Marekani, Israel na fedha za baadhi ya nchi za Kiarabu, imesema kuwa baada ya kumalizika vita dhidi ya kundi hilo Iraq inatakiwa kujiweka tayari kwa ajili ya njama mpya za Washington na washirika wake.
-
Hizbullah: Muqawama ndilo chaguo la pekee la Wapalestina
Nov 02, 2017 07:57Afisa wa ngazi ya juu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuna haja ya kuendeleza mapambano dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel na kusisitiza kuwa Wapalestina hawana chaguo jingine ghairi ya muqawama.