-
Sisitizo la kuendeleza muqawama katika mwaka wa 17 wa Intifadha ya al Aqsa
Sep 30, 2017 03:58Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS siku ya Alkhamisi ilitoa tamko na kusema kuwa, muqawama ni chaguo la kiistratijia la wananchi wa Palestina na ni haki ya wananchi hao kwa ajili ya kupambana na wavamizi wa ardhi zao.
-
HAMAS: Hakuna cha kuzungumzwa kuhusu silaha za muqawama
Sep 29, 2017 07:37Naibu Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesisitiza kwamba katika mazungumzo na harakati ya Fat-h, Hamas haikukubaliana na wazo la kuwapokonya silaha wanamuqawama na kwamba suala hilo halikujadiliwa katika mazungumzo yaliyopita wala halitojadiliwa katika mustakabali.
-
Hamas: Tutafungamana na chaguo la muqawama ili kufanikisha malengo ya wananchi wa Palestina
Sep 14, 2017 07:58Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesisitiza kuwa itaendelea kufungamana na chaguo la muqawama kama njia pekee ya kufanikisha malengo ya wananchi wa Palestina katika ardhi yenye uhuru na kujitawala.
-
Iran kuzidisha himaya na uungaji mkono kwa harakati za muqawama
Sep 03, 2017 07:21Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema taifa hili litaendelea kuyapa himaya na kuyaunga mkono makundi ya wanaharakati wa muqawama licha ya madola ya Magharibi kuitaka Tehran isiyaunge mkono makundi hayo.
-
Magaidi wa Daesh (ISIS) wajisalimisha kwa Hizbullah ya Lebanon
Aug 27, 2017 14:38Wapiganaji wenye silaha wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh (ISIS) wamejisalimisha kwa vikosi vya muqawama baada ya vikosi hivyo kuwakaribia magaidi hao katika eneo la mpaka wa pamoja wa Lebanon na Syria.
-
Mafanikio makubwa ya muqawama; kuongezeka kasi ya kuangamizwa kundi la kigaidi la Daesh (ISIS)
Aug 26, 2017 03:53Mwenendo wa kuliangamiza na kulitokomeza kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh umezidi kushika kasi kutokana na azma thabiti na mkakati madhubuti unaotekelezwa na mhimili wa muqawama katika mapambano na kundi hilo.
-
Harakati za Palestina zaonya kuhusu jinai za Wazayuni katika Msikiti wa Al Aqsa
Jul 18, 2017 15:43Harakati za mapambano ya kupigania ukombozi wa Palestina katika Ukanda wa Ghaza zimetahadharisha kuhusu jinai mpya zinazofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Msikiti wa Al Aqsa katika mji wa Quds unaokaliwa kwa mabavu.
-
Dunia yalaani hatua ya Israel kuufunga Msikiti wa al-Aqsa
Jul 15, 2017 12:56Nchi za Kiislamu duniani zinaendelea kulaani hatua ya utawala haramu wa Israel ya kuufunga Msikiti wa al Aqsa katika mji wa Quds Tukufu (Jerusalem) unaokaliwa kwa mabavu baada ya oparesheni ya Wapalestina dhidi wanajeshi wa Kizayuni karibu na msikiti huo.
-
HAMAS: Iran inaendelea kuunga mkono mapambano ya Palestina
Jul 09, 2017 07:39Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaendelea kuunga mkono mapambano ya wananchi wa Palestina na hakuna wakati ambao Tehran ilisitisha himaya na uungaji mkono wake huo.
-
Israel; hatari kuu ya ulimwengu wa Kiislamu
Jun 29, 2017 04:12Naibu Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Waislamu wa Kishia nchini Lebanon amesema kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel ndiyo hatari kuu kwa umma wa Kiislamu na kwamba kitendo cha baadhi ya nchi za Kiislamu cha kuwa na uhusiano na Israel ni hatari kubwa kwa Waislamu.