-
Israel imepeleka Ghaza maboksi yenye mafuvu na miili iliyonyofolewa ya wanawake Wapalestina
Feb 24, 2026 11:15Mbunge wa kujitegemea, ambaye pia ni kiongozi wa zamani wa chama cha Leba nchini Uingereza Jeremy Corbyn, ametoa simulizi za kutisha zilizotokana na maelezo ya mkurugenzi wa Hospitali ya Al-Shifa katika Ukanda wa Ghaza uliozingirwa, zinazobainisha kwa undani jinsi utawala wa kizayuni wa Israel ulivyopeleka katika eneo hilo masanduku kadhaa yenye mafuvu ya vichwa na mabaki ya Wapalestina yaliyokatwakatwa.
-
Licha ya vizuizi vikali vya Israel, Wapalestina laki moja wasali I'sha na Tarawehe Masjidul-Aqsa
Feb 21, 2026 11:07Licha ya vizuizi vikali vilivyowekwa na utawala wa Kizayuni wa Israel vya kuingia katika Msikiti wa Al-Aqsa, makumi ya maelfu ya Wapalestina jana usiku walihudhuria katika msikiti huo mtukufu kusali Sala za I'sha na Tarawehe wakati huu wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
Ripota wa UN kuhusu Palestina asema, licha ya kuandamwa hatasalimu amri, hatajiuzulu
Feb 21, 2026 02:36Francesca Albanese, ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa wa maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu, amesema hatajiuzulu wadhifa wake huo licha ya mashinikizo yanayotolewa dhidi yake na serikali za nchi kadhaa za Ulaya kutokana na matamshi yanayodaiwa kuwa ametoa dhidi ya utawala wa kizayuni wa Israel.
-
Viongozi wa Afrika watangaza mshikamano na watu wa Palestina
Feb 17, 2026 07:46Viongozi wa nchi za Afrika wametangaza mshikamano wao na watu wa Palestina na haki yao ya kujitawala.
-
"Ni muhali kufikia amani na Israel madhali inakiuka haki za Wapalestina"
Feb 16, 2026 10:17Waziri wa Mambo ya Nje na Wahamiaji wa Palestina, Varsen Aghabekian Shahin amesema kufikia amani na Israel "haiyumkiniki" madhali haki za Wapalestina zinakiukwa na utawala huo wa Kizayuni, akisisitiza kwamba sheria za kimataifa zinapasa kuzingatiwa, na uchukuaji wa hatua za upande mmoja lazima ukomeshwe.
-
Umoja wa Afrika: Mateso dhidi ya Wapalestina lazima yakomeshwe
Feb 15, 2026 02:50Mahmoud Ali Youssouf Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU) amesema kuwa, mauaji dhidi ya wananchi wa Palestina ni lazima yakomeshwe. Mahmoud Ali Youssouf alisema hayo jana (Jumamosi) wakati akiufungua mkutano wa kilele wa 39 wa umoja huo.
-
Palestina inavyotokomezwa kupitia ukoloni; Iran yalaani uamuzi wa Israel wa kunyakua Ukingo wa Magharibi
Feb 13, 2026 07:21Iran imelaani vikali uamuzi wa hivi karibuni wa utawala wa Israel wa kunyakua ardhi zaidi za Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu, ikisema kuwa hatua hiyo inalenga kupanua "ujenzi haramu wa vitongoji vya walowezi za Kizayuni" na kuimarisha ukaliaji mabavu na hatua kali za kiusalama dhidi ya Wapalestina na kuendelea "mauaji ya kimbari" huko Gaza.
-
Katika upeo wa unyama, Israel imetumia silaha 'zilizoyeyusha' maelfu ya Wapalestina Ghaza
Feb 12, 2026 02:32Uchunguzi uliofanywa na televisheni ya Al Jazeera ya Qatar umefichua kuwa, utawala wa kizayuni wa Israel umetumia silaha zilizopigwa marufuku kimataifa zenye joto kupindukia katika vita vya mauaji ya kimbari huko Ghaza, na kupelekea "kuyeyuka" maelfu ya miili ya Wapalestina.
-
Harakati ya BDS yalaani undumakuwili wa Human Rights Watch
Feb 09, 2026 10:09Kamati ya Kitaifa ya Palestina ya harakati inayopinga dhulma na ukandamizaji wa utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina BDS imelikosoa vikali shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch kwa kutoa ripoti za upendeleo zinazoakisi haki za Wapalestina, ikiwa ni pamoja na haki ya kurejea katika ardhi za mababu zao, na kudogosha ukiukwaji wa haki za Wapalestina wa Gaza unaofanywa na utawala wa Kizayuni.
-
Israel yaua Wapalestina 31 wakiwemo watoto 6 katika ukiukaji mpya wa usitishaji vita Ghaza
Jan 31, 2026 14:44Wapalestina wasiopungua 31, wakiwemo kwa uchache watoto sita, wameuawa shahidi katika mashambulizi ya kinyama yaliyofanywa na jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel tangu alfajiri ya leo hadi wakati huu katika Jiji la Ghaza na mji wa Khan Younis katika Ukanda wa Ghaza.