-
UNRWA: 90% ya Wapalestina Ghaza wanategemea msaada, wanapitisha siku kwa mlo mmoja
Nov 26, 2025 12:17Shirika la Umoja wa Mataifa la Kutoa Misaada na Ajira kwa Wakimbizi wa Palestina (UNRWA) limesema, hali ya kibinadamu katika Ukanda wa Ghaza ingali ni ya majanga licha ya kusitishwa mapigano, na kuonya kwamba vizuizi vinavyowekwa na utawala wa kizayuni wa Israel kwa uingizaji wa misaada vinaifanya hali ya eneo hilo isiweze kuboreka.
-
Baada ya Israel kuwaua Wapalestina wengine 24 Ghaza, HAMAS yataka wapatanishi, hasa US iingilie kati
Nov 23, 2025 07:05Jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel limefanya mashambulizi makali ya anga katika maeneo tofauti ya Ukanda wa Ghaza, na kuwaua shahidi Wapalestina wasiopungua 24, wakiwemo watoto, katika mwendelezo wa ukiukaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyofikiwa tangu wiki sita zilizopita kwenye eneo hilo la Palestina lililoteketezwa kwa vita.
-
Sababu za Ripota wa UN za kuonya kuhusu kuendelea Ulaya kuipa silaha Israel
Nov 22, 2025 02:24Umoja wa Mataifa umeonya kuhusu kuendelea nchi za Ulaya kuisheheneza silaha Israel licha ya kwamba kuna ushahidi wa kutosha na usiopingika wa jinsi utawala wa Kizayuni unavyotumia silaha hizo kufanya jinai na mauaji ya umati dhidi ya watu wasio na hatia.
-
Israel yafanya mashambulio ya kinyama Ghaza, yaua Wapalestina 28 na kujeruhi 77
Nov 20, 2025 06:09Wapalestina wasiopunguua 28 wameuawa shahidi katika wimbi jipya la mashambulizi ya kinyama yanayofanywa na jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel kwenye Ukanda wa Ghaza, yakiwa ni moja ya ukiukaji mkubwa zaidi wa makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyosimamiwa na Marekani na kuanza kutekelezwa mwezi uliopita wa Oktoba.
-
'Siku ya fedheha’: Afisa wa zamani wa haki za binadamu wa UN akosoa azimio la UNSC kuhusu Gaza
Nov 19, 2025 06:56Afisa wa ngazi ya juu wa zamani wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa amelaani hatua ya Baraza la Usalama la umoja huo ya kupitishaa azimio linalounga mkono mpango wa Marekani wa kuanzisha kikosi cha kimataifa cha kurejesha utulivu katika Ukanda wa Gaza uliozingirwa, akiitaja kura hiyo kuwa ni "siku ya fedheha" kwa chombo hicho cha dunia.
-
Jihadul-Islami: Muqawama hautaitambua Israel, hakutakuwa na suluhu bila Palestina kupata haki zake
Nov 16, 2025 02:29Mwakilishi wa harakati ya Jihadul-Islami ya Palestina hapa mjini Tehran amesema: "sisi katika mavuguvugu ya Muqawama wa Kiislamu hatutambui uwepo wa utawala wa Kizayuni na hatulazimiki kuutambua, hasa kwa vile utawala huu hautambui hata uwepo wa watu wa Palestina."
-
Kwa nini China na Russia zimepinga azimio lililopendekezwa na Marekani kuhusu Gaza?
Nov 16, 2025 02:26Russia na China ambazo ni wanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa zimetaka kufutwa kikamilifu "Tume ya Amani" kwenye matini ya rasimu iliyowasilishwa na Marekani kwenye baraza kuhusu Gaza.
-
Jumamosi, 15 Novemba 2025
Nov 15, 2025 02:39Leo ni Jumamosi 24 Mfunguo Nane Jamadul-Awwal 1447 Hijria mwafaka na 15 Novemba 2025 Miladia.
-
Maiti zingine 51 za Wapalestina waliouliwa shahidi na jeshi la kizayuni zagunduliwa Ghaza
Nov 14, 2025 07:43Timu za uokoaji za Palestina katika Ukanda wa Ghaza zimegundua na kufukua maiti zingine 51 za Wapalestina waliouliwa shahidi na jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel.
-
Maafa ya vita vya kinyama vya Israel yamepelekea Wapalestina 6,000 wa Ghaza kukatwa viungo
Nov 14, 2025 02:37Wizara ya Afya ya Palestina katika Ukanda wa Ghaza imetoa ripoti inayoonyesha kuwa, Wapalestina 6,000 wamekatwa viungo katika eneo hilo tangu utawala wa kizayuni wa Israael ulipoanzisha vita vya kinyama Oktoba 2023 ambavyo vimeendelea kwa muda wa miaka miwili.