-
Hamas: Netanyahu hana nia ya kufikia makubaliano ya usitishaji vita
Jul 15, 2025 04:52Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas imesema Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu hana azma kabisa ya kufikia makubaliano ya kusitisha mapigano, ili kuhitimisha kampeni ya mauaji ya halaiki inayoendelea katika Ukanda wa Gaza uliozingirwa.
-
Ripoti: Israel inatumia droni za kiraia kuwaua watoto wa Gaza
Jul 14, 2025 13:39Jeshi la Israel limekiri kutumia ndege zisizo na rubani za kiraia kushambulia maeneo ya Gaza, na kuua raia wa Kipalestina, aghalabu yao wakiwa watoto wadogo.
-
Wananchi wa Argentina waandamana kuliunga mkono taifa la Palestina
Jul 14, 2025 13:21Maandamano makubwa yamefanyika katika mji mkuu wa Argentina, Buenos Aires, huku maelfu ya wananchi wakikusanyika katika baadhi ya barabara kuu na nembo na vituo muhimu vya jiji hilo, kutangaza himaya na uungaji mkono wao kwa taifa madhulumu la Palestina.
-
Je, ushirikiano wa serikali za Magharibi na Wazayuni katika mauaji ya kimbari ya Wapalestina una kiwango na mpaka?
Jul 14, 2025 11:46Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) limetangaza katika indhari liliyotoa hivi karibuni kwamba hali ya huduma za afya katika Ukanda wa Ghaza imefikia kiwango cha maafa.
-
Polisi UK yakamata makumi ya watu kwa kushiriki maandamano ya kuiunga mkono Palestina
Jul 13, 2025 07:06Polisi wa Uingereza imewakamata makumi ya wanaharakati wanaoiunga mkono Palestina wakati wa maandamano mapya ya kupinga marufuku ya vuguvugu la 'Palestine Action', kundi linalojulikana kwa maandamano yake dhidi ya makampuni ya silaha yenye uhusiano na Israel.
-
Jinai ya kutisha; Israel yaua shahidi Wapalestina 150 Gaza
Jul 13, 2025 05:32Wapalestina zaidi ya 150 wameuawa shahidi katika maeneo mbalimbali ya Ukanda wa Gaza, huku eneo hilo la pwani likishuhudia siku yake mbaya zaidi tangu mwezi Mei, wakati utawala wa Israel uliposhadidisha mauaji yake ya kimbari dhidi ya eneo hilo.
-
Wabunge 60 wa UK waitaka London ilitambue taifa la Palestina
Jul 12, 2025 16:20Kufuatia mpango tata wa Israel wa kuwahamisha kwa nguvu wakazi wa Gaza na kuwapeleka Rafah, takriban wabunge 60 wa Uingereza wameitaka serikali ya London kulitambua rasmi taifa la Palestina.
-
Raia wa US apigwa hadi kufa na walowezi wa Kizayuni Ukingo wa Magharibi
Jul 12, 2025 13:11Walowezi wa Israel wamempiga hadi kufa kijana mmoja raia wa Marekani katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan unaokaliwa kwa mabavu, kwa mujibu wa familia yake na mashirika ya kutetea haki za binadamu.
-
Uhispania na Ireland kujiunga na nchi zaidi ya 20 zitakazochukua 'hatua madhubuti' dhidi ya Israel
Jul 11, 2025 16:45Uhispania na Ireland zitajiunga na zaidi ya nchi 20 zitazokutana katika mji mkuu wa Colombia, Bogota wiki ijayo kutangaza "hatua madhubuti" dhidi ya ukiukaji wa sheria za kimataifa unaofanywa na utawala wa kizayuni wa Israel.
-
Upeo wa ukatili; Israel yaua Wapalestina zaidi ya 80 Gaza ndani ya saa 24
Jul 11, 2025 02:54Mashambulizi ya Israel katika maeneo mbali mbali huko Gaza yameua shahidi watu wasiopungua 82 tangu alfajiri ya jana, kwa mujibu wa Wizara ya Afya ya Gaza, wakati huu ambapo mazungumzo yanaendelea ya kusitisha mapigano hayo.