-
Unajua kwa nini Marekani imemuwekea vikwazo Ripota Maalumu wa UN kuhusu Maeneo ya Palestina Yanayokaliwa kwa Mabavu?
Jul 11, 2025 02:26Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Marco Rubio, alitangaza Jumatano, Julai 9, kwamba atamuwekea vikwazo Francesca Albanese, Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa katika Maeneo ya Palestina Yanayokaliwa kwa Mabavu, kwa kile alichokiita "juhudi zisizo halali zinazohusiana na uchunguzi wake kuhusu vita vya Israel dhidi ya watu wa Gaza" na eti kwa kuchukua "hatua dhidi ya maafisa wa Marekani na Israel."
-
Al-Qassam yamwangamiza askari wa Kizayuni baada ya kutofanikiwa kumkamata mateka
Jul 10, 2025 13:10Brigedi za Izzuddinul-Qassam, tawi la kijeshi la Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS limetangaza kuwa limelazimika kumuangamiza mwanajeshi mmoja wa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel katika mji wa Khan Younis, kusini mwa Ukanda wa Ghaza baada ya mazingira kwenye medani ya mapambano kutoruhusu kumkamata mateka.
-
HAMAS: Ghaza haitasalimu amri; Muqawama ndio utakaotoa masharti
Jul 10, 2025 07:35Kiongozi mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS Izzat al-Rishq amesema, Ghaza haitasalimu amri, na ni Muqawama ndio utakaotoa masharti, si utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Kwa nini njama za utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina zimeshindwa licha ya kuzingirwa Gaza?
Jul 09, 2025 02:35Licha ya kuendelea mzingiro wa Gaza na mashambulizi ya utawala wa Kizayuni dhidi ya wananchi wa Palestina, lakini makundi ya muqawama ya Palestina yanaendelea kusimama kidete na kukabiliana na njama za Wazayuni.
-
Jeshi la Israel lakiri askari wake 5 wameangamizwa, 14 wamejeruhiwa Ghaza
Jul 08, 2025 12:22Jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel limetangaza kuwa askari wake watano wameuawa na wengine 14 wamejeruhiwa katika mapigano kaskazini mwa Ukanda wa Ghaza.
-
Rais wa Brazil ailaani waziwazi Israel kwa mauaji ya kimbari ya Ghaza katika kikao cha BRICS
Jul 06, 2025 19:28Rais Luiz Inacio Lula da Silva wa Brazil amesema dunia lazima ichukue hatua kukomesha kile alichokitaja kama "mauaji ya kimbari" yanayofanywa Israel huko Ghaza.
-
Hamas: Muqawama utaendelea kukabiliana na mashambulizi ya Israel
Jul 01, 2025 12:25Afisa wa ngazi ya juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) ameonya kuwa kuendelea mashambulizi na hujuma za Israel kunazidisha mapambano na muqawama wa wananchi wa Palestina dhidi ya maghasibu Wazayuni.
-
"Kuuawa viongozi wa Muqawama kunaimarisha irada ya Wapalestina"
Jun 09, 2025 02:49Harakati ya Jihadul Islami ya Palestina imelaani vikali mauaji ya Israel dhidi ya afisa mashuhuri wa Muqawama na watu wengine 30 katika mji wa Gaza na kusisitiza kuwa, mauaji hayo yanayolenga viongozi wa mrengo wa mapambano kamwe hayatadhoofisha uthabiti na azma ya wananchi wa Palestina.
-
Kwa nini mashinikizo dhidi ya Netanyahu hayafanyi kazi?
Jun 04, 2025 11:02Mauaji ya Wapalestina wanaoishi Gaza yanayofanywa na utawala wa Kizayuni yangali yanaendelea, huku nchi na jumuiya mbalimbali za kimataifa zikitoa wito wa kukomeshwa mauaji hayo mara moja.
-
Israel yamjibu Macron: Kutambuliwa Palestina kutasalia kwenye karatasi tu
May 31, 2025 02:22Waziri wa Vita wa Israel, Israel Katz amemsuta na kumkejeli Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, ambaye alisema mapema jana kwamba, kutambuliwa kwa taifa la Palestina, kwa masharti, ni "wajibu wa kimaadili."