-
Iran yakosoa vikali uingiliaji wa nchi za Magharibi katika kazi za Baraza la Haki za Kibinadamu UN
Mar 19, 2025 04:15Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Ofisi ya Umoja wa Mataifa mjini Geneva amezikosoa vikali baadhi ya nchi za Magharibi kwa kutumia vibaya taasisi za Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa na kusisitiza kuwa, nchi hizo zinataka kuingiza siasa katika masuala ya haki za binadamu dhidi ya Iran kwa kupuuza masuala ya kimsingi ya haki za binadamu ukiwemo mgogoro wa Palestina.
-
Mwakilishi wa Palestina UN: Israel inaendeleza sera za mauaji ya kimbari
Mar 16, 2025 02:49Mwakilishi wa Kudumu wa Palestina katika Umoja wa Mataifa ametuma barua kwa maafisa wa kimataifa akikemea jinai zinazoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Paletina.
-
Hamas yalaani marufuku ya pamoja ya US na EU dhidi ya al Aqsa TV
Mar 15, 2025 14:37Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imelaani uamuzi uliochukuliwa na Marekani na Umoja wa Ulaya wa kupiga marufuku matangazo ya televisheni ya al Aqsa.
-
Waandamanaji New York washinikiza kuachiliwa Mahmoud Khalil
Mar 14, 2025 02:30Waandamanaji wanaoiunga mkono Palestina walikusanyika nje ya mahakama ya Manhattan jijini New York nchini Marekani, wakitaka mwanaharakati wa Kipalestina, Mahmoud Khalil aachiliwe huru.
-
Ripoti: Israel inawaua Wapalestina 3 huko Gaza kila baada ya saa 24
Mar 13, 2025 07:38Israel imewaua Wapalestina 150 kwa kutumia ndege zisizo na rubani, wadunguaji au njaa kama silaha tangu ilipofikia makubaliano ya kusimamisha mapigano na Harakati ya Mapambano ya Palestina Hamas Januari 19 mwaka huu.
-
Wanawake wa Palestina wanalishwa futari zilizooza kwenye jela za Israel
Mar 11, 2025 11:35Mateka wa Kipalestina wanaoshikiliwa kidhulma katika jela za Israel ikiwemo ile jela ya Damon wanaishi katika mateso makubwa yasiyoelezeka hasa ndani ya mwezi huu mtukufu wa Ramadhani ikiwa ni pamoja na kulazimishwa kula vyakula vilivyooza wakati wa futari na kutangaziwa nyakati sizo za wakati wa daku na futari.
-
Iran yalaani kufutwa mkutano wa Geneva wa kuijadili Palestina
Mar 10, 2025 11:21Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baghaei, amekosoa vikali uamuzi wa Uswisi wa kufuta Kongamano la Hati ya Geneva kuhusu Palestina.
-
Araghchi: Kuundwa nchi moja ya kidemokrasia ndiyo suluhu ya kadhia ya Palestina
Mar 08, 2025 07:02Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi amesisitiza tena msimamo wa Tehran wa kupinga eti 'suluhisho la mataifa mawili' kuwa njia ya kupata haki za Wapalestina na kusisitiza kwamba, uungaji mkono usioyumba wa Iran kwa kadhia ya Palestina bado upo thabiti.
-
Askari wa Israel wavamia misikiti mjini Nablus na kuzuia Swala ya Ijumaa
Mar 07, 2025 11:01Vikosi vya jeshi la Israel vimevamia misikiti kadhaa katika mji mkongwe wa Nablus, eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu, na kuzuia kuswaliwa Swala ya Ijumaa.
-
Jeshi la Israel launda kifaa cha AI cha kuwajasisi Wapalestina
Mar 07, 2025 10:57Uchunguzi mpya umefichua kuwa, kitengo cha ujasusi wa kielektroniki cha jeshi la Israel cha 8200 kimetumia mkusanyiko mkubwa wa mawasiliano yaliyonaswa kutengeneza chombo cha kijasusi cha Akili Mnemba (AI) ambacho modeli yake inashabihiana na ChatGPT, kwa lengo la kuwachunguza na kuwafanyia ujasusi wananchi wa Palestina.