-
Mtengeneza filamu mashuhuri ya Palestina iliyoshinda Oscar apigwa na kukamatwa na askari wa Israel
Mar 25, 2025 08:17Hamdan Ballal, mtengeneza filamu mwenza wa Kipalestina wa filamu iliyoshinda tuzo ya Oscar iitwayo Hakuna Ardhi Nyingine (No Other Land) amekamatwa na wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu baada ya kupigwa na kujeruhiwa vibaya sana na walowezi wa Kizayuni. Hayo yameripotiwa na Yuval Abraham aliyeshirikiana naye kutengeneza filamu hiyo.
-
Jeshi katili la Israel laendelea kumwaga damu za Wapalestina Gaza
Mar 24, 2025 23:21Wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel wamewaua shahidi Wapalestina wengine 17 katika mashambulizi ya alfajiri ya leo katika Ukanda wa Gaza, siku moja baada ya kuua shahidi Wapalestina zaidi ya 60 akiwemo ripota wa Al Jazeera, Hossam Shabat katika ukanda huo.
-
Siku ya saba ya uvamizi wa Israel wa Ghaza; makumi wauawa na kujeruhiwa
Mar 24, 2025 07:21Utawala wa wa Kizayuni wa Israel Israel unaendelea kufanya jinai na mashambulizi ya anga katika maeneo mbalimbali ya Ukanda wa Ghaza ambapo tangu asubuhi ya leo hadi wakati tunaandaa taarifa hii, makumi ya Wapalestina wamekuwa wameshauwa shahidi na kujeruhiwa, leo ikiwa ni siku ya saba ya tangu kuanza wimbi jipya la jinai za utawala wa Kizayuni huko Ghaza.
-
Israel yapigwa na makombora kutoka Yemen, ving'ora vyahanikiza
Mar 23, 2025 07:21Vikosi vya Ulinzi vya Yemen vimevurumisha makombora kuelekea katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na Israel, na kuwatia kiwewe na hofu Wazayuni; huku safari za ndege zikisimamishwa Tel Aviv.
-
Rais wa Mexico ampokea rasmi balozi mpya wa Palestina
Mar 22, 2025 23:17Rais wa Mexico, Claudia Sheinbaum amepokea rasmi hati za utambulisho za Balozi wa Palestina Nadya R. H. Rasheed katika Ikulu ya Mexico City.
-
Netanyahu: Mashambulio yalioua watoto 174 Gaza ni mwanzo tu
Mar 19, 2025 23:40Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu ametangaza kushadidi mashambulio mabaya dhidi ya Gaza, akionya kwamba mashambulizi ya hivi karibuni ya anga, ambayo yaliua watoto wasiopungua 174 katika ukanda huo, ni mwanzo tu wa uchokozi mkubwa zaidi dhidi ya Wapalestina.
-
Iran yakosoa vikali uingiliaji wa nchi za Magharibi katika kazi za Baraza la Haki za Kibinadamu UN
Mar 19, 2025 00:45Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Ofisi ya Umoja wa Mataifa mjini Geneva amezikosoa vikali baadhi ya nchi za Magharibi kwa kutumia vibaya taasisi za Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa na kusisitiza kuwa, nchi hizo zinataka kuingiza siasa katika masuala ya haki za binadamu dhidi ya Iran kwa kupuuza masuala ya kimsingi ya haki za binadamu ukiwemo mgogoro wa Palestina.
-
Mwakilishi wa Palestina UN: Israel inaendeleza sera za mauaji ya kimbari
Mar 15, 2025 23:19Mwakilishi wa Kudumu wa Palestina katika Umoja wa Mataifa ametuma barua kwa maafisa wa kimataifa akikemea jinai zinazoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Paletina.
-
Hamas yalaani marufuku ya pamoja ya US na EU dhidi ya al Aqsa TV
Mar 15, 2025 11:07Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imelaani uamuzi uliochukuliwa na Marekani na Umoja wa Ulaya wa kupiga marufuku matangazo ya televisheni ya al Aqsa.
-
Waandamanaji New York washinikiza kuachiliwa Mahmoud Khalil
Mar 13, 2025 23:00Waandamanaji wanaoiunga mkono Palestina walikusanyika nje ya mahakama ya Manhattan jijini New York nchini Marekani, wakitaka mwanaharakati wa Kipalestina, Mahmoud Khalil aachiliwe huru.