-
Hujuma mpya za Israel zaua shahidi Wapalestina 70 Rafah, Khan Younis
Oct 17, 2023 10:24Wapalestina wasiopungua 70 wameuawa shahidi katika mashambulizi mapya ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika miji ya Rafah na Khan Younis, kusini mwa eneo la Ukanda wa Gaza, huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
-
Abdollahian: Sera za Marekani zinachochea moto wa vita Gaza
Oct 17, 2023 10:05Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema sera haribifu za Washington na uungaji mkono wake kwa hatua ya utawala wa Kizayuni ya kuwashambulia raia katika Ukanda wa Gaza ndiyo sababu kuu ya kushadidi na kupanuka vita katika eneo hilo la pwani ambalo liko chini ya mzingiro.
-
Uturuki kuwasilisha OIC mpango pendekezwa wa kutatua mgogoro wa Gaza
Oct 17, 2023 08:59Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki ametangaza kuwa atawasilisha katika kikao cha Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC mpango uliopendekezwa na nchi yake kwa ajili ya kutatua mgogoro wa Gaza
-
Kiongozi Mkuu wa Iran: Jinai za Gaza zisiposimamishwa, hakuna atakayeweza kuwazuia Waislamu na Wanamuqawama
Oct 17, 2023 08:31Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema: wananchi wa mataifa ya Kiislamu na hata watu wasio Waislamu duniani wamekasirishwa sana na jinai zinazoendelea kufanywa na utawala unaoikalia Quds kwa mabavu, na iwapo unyama na ushenzi huo utaendelea Waislamu duniani na vikosi vya Muqawama wataishiwa na subira na hakuna atakayeweza kuwazuia.
-
Balozi wa Israel atimuliwa Colombia kulalamikia jinai za Wazayuni Ukanda wa Ghaza
Oct 17, 2023 02:32Duru mbalimbali za habari zimetangaza usiku wa kuamkia leo Jumanne kwamba, nchi ya Colombia ya Amerika ya Latini imemtimua balozi wa utawala wa Kizayuni wa Israel ikiwa ni kulalamikia jinai za utawala huo dhidi ya wananchi wasio na ulinzi wa Ghaza.
-
Hamas: Nchi zinazounga mkono mashambulizi ya Israel zinahusika katika mauaji ya watoto na wanawake
Oct 17, 2023 00:17Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) ilisema jana Jumatatu kuwa, nchi zinazounga mkono uvamizi wa Israel katika hujuma yake inayoendelea dhidi ya Ukanda wa Gaza unaozingirwa zinahusika katika mauaji ya watoto, wanawake na raia.
-
Velayati: Kusimama kidete muqawama ndio njia sahihi ya kufikia kilele cha ushindi
Oct 16, 2023 10:16Mshauri wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika masuala ya kimataifa amesema kuwa, kusimama kidete muqawama ndio njia sahihi ya kufikia kilele cha ushindi.
-
Raisi: Inapasa kuwabebesha dhima wanaonyamazia kimya jinai za Israel
Oct 15, 2023 23:38Rais Ebrahim Raisi wa Iran amesema kuliunga mkono taifa linalodhulumiwa la Palestina ni katika misingi ya sera za Jamhuri ya Kiislamu na kuongeza kuwa, wanaonyamazia kimya jinai za Israel watabeba mas'ulia mbele ya Mwenyezi Mungu, mienendo yao na historia.
-
Ni mbwa, si mtoto.. Mwandishi habari wa Marekani afichua uongo wa Netanyahu, madai ya Hamas kuua watoto
Oct 15, 2023 22:59Mwandishi wa habari wa Marekani, Jackson Hinkle, meifichua uwongo wa picha iliyodaiwa ni ya mtoto aliyeungua moto iliyochapishwa na Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, aliyesema kwamba ilikuwa ya mtoto wa Kiisraeli aliyechomwa moto na wapiganaji wa Harakati ya mapambano ya Kislamu ya Palestina (Hamas).
-
Wakenya wawasha mishumaa kuonyesha mshikamano na Wapalestina
Oct 15, 2023 07:58Wananchi wa Kenya wamekusanyika na kuwawasha mishumaa katika mji mkuu wa nchi hiyo, Nairobi kuonyesha mshikamano wao na wananchi wa Palestina. Mashirika yaliyoandaa shughuli hiyo ni pamoja na Kenyans 4 Palestine, The Pan African Palestine Solidarity Network (PAPSN) na podkasti ya 'Until Everyone is Free.'