-
Mpango wa UK wawaacha bila makazi wahanga wa mauaji ya kimbari Rwanda
Sep 01, 2022 03:06Wahanga wa mauaji ya kimbari nchini Rwanda waliofurushwa katika mabweni walikokuwa wakiishi kutokana na mpango tata wa wakimbizi wa Uingereza, wanalalamika kuwa wameachwa bila pahala pa kuishi, licha ya mabweni hayo kusalia bila watu.
-
Upinzani DRC wakosoa vikali mikakati ya Rais Tshisekedi ya kukabiliana na Rwanda
Aug 06, 2022 22:29Wapinzani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamemlaumu vikali Rais Felix Tshisekedi na mikakati yake ya kuamiliana na Rwanda kufuatia ripoti iliyotolewa hivi karibuni na wataalamu wa Umoja wa Mataifa inayoeleza kwamba serikali ya Kigali imekuwa ikilisaidia na kuliunga mkono kundi la waasi wa M23 linalopigana na serikali ya Kinshasa.
-
Wataalamu wa UN: Rwanda inawaunga mkono waasi wa M23 Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Aug 05, 2022 03:43Vikosi vya jeshi la Rwanda viliwashambulia askari ndani ya ardhi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na vililisaidia na kulipatia na silaha kundi la waasi wa M23.
-
Kagame asema atagombea tena urais wa Rwanda 2024
Jul 09, 2022 22:16Rais Paul Kagame wa Rwanda, ambaye amekuweko madarakani tangu yalipohitimishwa mauaji ya kimbari nchini humo mwaka 1994, amedokeza kuwa atagombea tena urais katika uchaguzi unaotazamiwa kufanyika 2024.
-
Waasi wa M23: Makubaliano ya DRC na Rwanda hayatuhusu
Jul 08, 2022 05:34Kundi la waasi wa M23 linaloendesha harakati zake mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limesema halitaheshimu wala kufungamana na makubaliano ya usitishaji vita yaliyoafikiwa Jumatano baina ya viongozi wa DRC na Rwanda.
-
DRC na Rwanda zakubaliana kupunguza mivutano kwa sababu ya waasi wa M23
Jul 07, 2022 06:55Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC na Rwanda zimekubaliana kutekeleza "mchakato wa kupunguza mvutano" baina yao kufuatia mazungumzo ya siku moja yaliyofanywa na marais wa nchi hizo mbili kwa upatanishi wa rais wa Angola.
-
Marais wa Rwanda na DRC kufanya mazungumzo Luanda chini ya upatanishi wa rais wa Angola
Jul 05, 2022 22:01Serikali ya Angola imesema, marais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Rwanda wanakutana leo Jumatano kwa mazungumzo ya kutafuta suluhu baina yao yatakayofanyika katika mji mkuu wa nchi hiyo Luanda kwa upatanishi wa Rais Joao Lourenco.
-
Ijumaa tarehe Mosi Julai 2022
Jun 30, 2022 20:31Leo ni Ijumaa tarehe Mosi Dhulqaada 1443 Hijria sawa na tarehe Mosi Julai 2022.
-
EAC yataka waasi wa M23 waondoke mara moja mashariki mwa DRC
Jun 21, 2022 03:32Jumuiya ya Afrika Mashariki imelitaka kundi la waasi la M23 liondoke mara moja katika mji wa Bunagana unaodhibitiwa na wanamgambo hao, huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
DRC yafunga mpaka na Rwanda baada ya askari wake kuuawa
Jun 18, 2022 07:57Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imetangaza kufunga mpaka wake na Rwanda baada ya askari wa jeshi la DRC kuuawa kwa kupigwa risasi wakati jeshi hilo lilipowashambulia askari wanaolinda mpaka ndani ya ardhi ya Rwanda.