-
Kikao cha utangulizi cha wakuu wa nchi za Kiarabu, uchochezi dhidi ya Iran
Apr 13, 2018 21:53Huku akikanusha tuhuma zilizotolewa hivi karibuni dhidi ya Iran kupitia taarifa ya kikao cha nane cha kamati ya pande nne ya Kiarabu huko Saudia, Bahram Qassemi, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa tuhuma hizo hazina msingi na kwamba ni za dharau.
-
Nchi zinazoizingira Qatar zakariri madai yao kwa Doha kama sharti la kufungua upya mahusiano
Apr 13, 2018 02:53Kwa mara nyingine nchi nne za Kiarabu zainazoizingira Qatar ambazo ni Saudi Arabia, Bahrain, Imarati na Misri, zimekariri masharti yao 13 kwa serikali ya Doha kama njia ya kufungua upya uhusiano wao na nchi hiyo.
-
Qassemi: Wasaudia sawa na Wazayuni wamekuwa nembo za wavamizi na watenda jinai Mashariki ya Kati
Apr 11, 2018 22:03Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, watawala wa hivi sasa wa Saudi Arabia wamekuwa ni nembo ya uvamizi na kutenda jinai Mashariki ya Kati sawa kabisa na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Alimu mkubwa Tunisia: Fatwa za mamufti wa Kiwahabi, zinalenga kuusambaratisha Uislamu
Apr 11, 2018 00:08Alimu mmoja wa ngazi ya juu wa Kiislamu nchini Tunisia, amesema kuwa fatwa za upotoshaji za mamufti wa Saudia, zinaelekea kuuangamiza umma wa Kiislamu.
-
Saudia inapanga kuigeuza Qatar kisiwa na jalala la takataka za nyuklia
Apr 10, 2018 12:25Saudi Arabia inapanga kuanzisha mradi wa ujenzi wa mfereji kwenye mpaka wake wa pamoja wa ardhini na Qatar ambao utaigeuza nchi hiyo ndogo ya Kiarabu katika Ghuba ya Uajemi kuwa kisiwa.
-
Wimbi la upinzani wa kuuziwa silaha Saudi Arabia huko Ufaransa
Apr 10, 2018 07:55Malalamiko ya kutaka kusitishwa kuuziwa silaha Saudi Arabia yameshadidi nchini Ufaransa sambamba na safari ya Muhammad bin Salman, mrithi wa kiti cha ufalme wa Saudia katika nchi hiyo ya bara Ulaya.
-
Wasomi wa Kiislam Nepal: Aal-Saud waache kutumia vibaya na kisiasa maeneo ya Waislamu
Apr 09, 2018 09:34Wasomi wakubwa wa Kiislamu nchini Nepal wameulaani utawala wa kifalme wa Aal-Saud nchini Saudia kwa hatua yake ya kutumia kisiasa na kwa malengo yao binafsi ibada ya Hijjah na maeneo matukufu ya Waislamu.
-
Askari wa Saudia wanaoshiriki vita Yemen wachoshwa na mienendo hasi ya Bin Salman
Apr 07, 2018 22:24Kufuatia kuzorota usalama wa maeneo ya mpakani ya Saudia kutokana na vita vya muungano vamizi wa nchi za Kiarabu unaoongozwa na Saudia dhidi ya Yemen, askari wa Saudia wanaolinda mpaka wameonyesha kukerwa na mienendo mibaya ya Mohammad Bin Salman kwa kutuma video za malalamiko katika mitandao ya kijamii.
-
Marekani yaafiki kuiuzia Saudia silaha licha ya mauaji ya Wayemeni
Apr 06, 2018 03:14Washington imekubali kuiuzia Riyadh mifumo 180 ya mizinga yenye thamani ya dola bilioni 1.31 ikiwa ni katika mwendelezo wa Marekani wa kuiuzia Saudia silaha za mabilioni ya dola.
-
Hujuma ya tatu ya Wayemen iliyolenga Shirika la Aramco, mwaka mgumu wa kivita kwa Saudia
Apr 05, 2018 21:53Vikosi vya Jeshi la Yemen na Kamati za Wananchi kwa mara nyingine vimevurumisha makombora ya balistiki ya Badr ambayo yamelenga kwa mafanikio vituo vya kuzalisha mafuta ya petroli vya Shirika la Aramco la Saudi Arabia katika mji wa Jizan ulio kusini magharibi mwa Saudia.