-
Mbunge wa Kizayuni afichua: 2023 Saudia na Israel zitasaini mkataba wa kuanzisha uhusiano rasmi
Dec 13, 2022 22:56Mbunge wa chama cha Likud katika Bunge la utawala haramu wa Kizayuni wa Israel amesema, kwa kuzingatia mazungumzo yaliyofanyika, inatarajiwa kuwa makubaliano ya kuanzishwa uhusiano wa kawaida kati ya utawala huo na Saudi Arabia yatasainiwa mwaka ujao wa 2023.
-
Saudia yakosolewa kwa kuzima sauti ya adhana kwa ajili ya hafla za ufuska
Dec 07, 2022 22:51Licha ya ukandamizaji wa kimfumo wa utawala wa Saudia dhidi ya wale wanaokosoa mwelekeo wa kisiasa na kijamii wa utawala huo unaolazimishwa kwa watu kwa mabavu, sauti zimeanza kupazwa nchini humo dhidi ya hafla na sherehe za ufuska na ufisadi zinazoandaliwa na kile kinachoitwa Mamlaka Kuu ya Burudani katika Ufalme huo.
-
Umoja wa Mataifa wakosoa vikali hukumu za kukatwa watu vichwa Saudi Arabia
Nov 22, 2022 23:09Mmoja wa wasemaji wanaohusika na haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa ameelezea masikitiko yake kuhusu utekelezwaji wa hukumu za vifo kwa kukata watu vichwa nchini Saudi Arabia.
-
Bin Salman ajibiwa: Kuvunjiwa heshima Haram Mbili Takatifu haliwi tena suala la ndani la Saudia
Nov 08, 2022 04:08Wanaharakati wa mitandao ya kijamii wamemjibu Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Saudi Arabia aliyedai kwamba hakuna mtu yeyote mwenye haki ya kuingilia masuala ya ndani ya nchi hiyo kwa kumueleza kuwa kutusi na kuvunjia heshima nchi ambayo ndani yake kuna Haram mbili za Makka na Madina haliwi suala la ndani la Saudia.
-
Msururu wa hukumu za vifo na kunyonga watu kwa halaiki; rekodi ya jinai aliyojiwekea Bin Salman
Nov 07, 2022 05:40Shirika la Haki za Kibinadamu la Saudi Arabia lenye makao yake Ulaya limefichua kuwa viongozi wa utawala wa Riyadh wametoa hukumu ya kifo kwa wafungwa 15 walioshtakiwa kwa masuala ya kiitikadi, na kwamba kwa kutolewa hukumu hizo, idadi ya watu walio hatarini kunyongwa nchini humo imefika 53, wanane miongoni mwao wakiwa ni vijana chipukizi na watoto wadogo.
-
Iran yajibu uvumi wa gazeti la Marekani kuhusu kuishambulia Saudia
Nov 02, 2022 23:11Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amejibu uvumi ulioenezwa na gazeti la Marekani la Wall Street Journal lililodai kuwa kuna uwezekano Iran ikashambulia baadhi ya maeneo ya Saudi Arabia na kusema kuwa hayo ni madai chapwa yasiyo na msingi wowote.
-
Walebanon wataka kutimuliwa balozi wa Saudi Arabia mjini Beirut
Nov 02, 2022 10:09Wananchi wa Lebanon wametoa mwito wa kutimuliwa nchini humo balozi wa Saudi Arabia wakimtuhumu kwamba, amekuwa akiingilia masuala ya ndani ya nchi hiyo.
-
Hizbullah: Saudia na Marekani zinakwamisha uchaguzi wa Rais wa Lebanon
Oct 25, 2022 07:29Afisa mwandamizi wa Harakati ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon amesema balozi za Saudi Arabia na Marekani jijini Beirut zimekula njama na kuweka vizingiti vya kila aina ili kukwamisha uchaguzi wa rais, huku ikiwa imesalia wiki moja tu kabla ya kumalizika muhula wa Rais Michel Aoun wa nchi hiyo.
-
Sanders aitaka Marekani iondoe askari wake Saudia, iache kuiuzia silaha
Oct 08, 2022 03:20Seneta wa kujitegemea aliyekuwa pia mgombea uteuzi wa kuwania urais wa Marekani kwa tiketi ya chama cha Democratic ametoa wito wa kuondolewa wanajeshi wa Marekani nchini Saudi Arabia na kukomeshwa kwa misaada ya kijeshi kwa Ufalme wa kihafidhina wa nchi hiyo kwa sababu ya kupunguza uzalishaji wa mafuta.
-
Yemen: Hakutakuwa na usitishaji vita hadi haki za watu wa Yemen zipatikane
Oct 06, 2022 23:04Waziri Mkuu wa Serikali ya Uokovu wa Kitaifa ya Yemen ameutaja muungano vamizi unaoongozwa na Saudi Arabia na Umoja wa Mataifa kuwa zinahusika katika kufeli kwa usitishaji vita huko Yemen.