-
Magaidi 62 wa Al Shabab waangamizwa Somalia
Dec 18, 2018 03:51Jeshi la Kitaifa la Somalia limetangaza kuwa magaidi 62 wa Al Shabab wameangamizwa katika oparesheni iliyofanyika kwenye eneo la Gandarsh katika jimbo la Banaadir la kusini mwa nchi hiyo.
-
Jeshi la Somalia na AU zafanya operesheni ya pamoja dhidi ya al Shabab
Dec 17, 2018 11:52Mkuu wa mipango ya opereshenei ya kikosi cha Umoja wa Afrika cha kulinda amani Somalia (AMISOM) amesema kuwa, askari wa kikosi hicho na wale wa serikali wanaendesha kwa pamoja operesheni ya kupambana na magaidi wa al Shabab kusini mwa Somalia.
-
Amisom: Hatujahusika na kukamatwa kamanda wa zamani wa al-Shabaab
Dec 15, 2018 04:07Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia, Amisom kimekanusha madai kuwa kilihusika katika operesheni ya kumtia mbaroni aliyekuwa Naibu Kamanda wa kundi la kigaidi na ukufurishaji la al-Shabaab na pia msemaji wa zamani wa genge hilo la ukufurishaji, Mukhtar Robow Abu Mansur.
-
Nchi za Afrika zataka msaada wa UN kuituliza Somalia
Dec 14, 2018 03:19Nchi wanachama wa Umoja wa Afrika zimesema zitaomba uungaji mkono wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuiwezesha Tume ya Umoja wa Afrika nchini Somalia AMISOM kutuliza hali ya Somalia.
-
Ghasia Somalia baada ya kamanda wa zamani wa al-Shabaab kukamatwa
Dec 13, 2018 10:27Watu wanne wameuawa nchini Somalia katika ghasia zilizoibuka baada ya kukamatwa aliyekuwa Naibu Kiongozi wa kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab na pia msemaji wa zamani wa genge hilo la ukufurishaji, Mukhtar Robow Abu Mansur.
-
Bunge la Somalia labatilisha hoja ya kutokuwa na imani na Rais
Dec 12, 2018 04:11Bunge la Somalia limebatilisha hoja iliyowasilishwa na baadhi ya wabunge waliotaka kupigiwa kura ya kutokuwa na imani na Rais wa nchi hiyo, Mohammed Abdullahi Farmajo.
-
Maandamano yafanyika Somalia kupinga kuvuliwa madaraka Rais Farmajo
Dec 11, 2018 04:38Wafuasi wa Rais Mohammed Abdullahi Farmajo wa Somalia wamefanya maandamano katika mji mkuu Mogadishu, kupinga kitendo cha wabunge kuwasilisha hoja bungeni ya kutaka kupiga kura ya kutokuwa na imani na rais huyo.
-
Mashambulio ya Marekani yaua watu tisa Somalia wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa Al-Shabab
Dec 02, 2018 11:16Jeshi la Marekani limearifu kuwa limefanya shambulio la anga huko Somalia na kuuwa watu tisa. Jeshi hilo limedai katika taarifa mbele ya vyombo vya habari kuwa jeshi hilo mapema leo lilishambulia eneo moja huko Somalia na kuuwa wanamgambo tisa wa kundi la al Shabab.
-
Mripuko katika mji mkuu wa Somalia waua watu wanane na kujeruhi wengine 10
Nov 26, 2018 12:17Jeshi la polisi nchini Somalia limetangaza habari ya kuuawa na kujeruhiwa watu wasiopungua 18 baada ya gari lililokuwa limetegwa mabomu kuripuka mjini Mogadishu leo Jumatatu.
-
Magaidi wa Al Shabab waua watu 10 katika hujuma mpya Somalia
Nov 26, 2018 04:43Magaidi wakufurishaji wa kundi la Al Shabab nchini Somalia wameshambulia kituo kimoja cha mafunzo ya Kiislamu kati mwa nchi hiyo na kumuua mhubiri na watu wengine tisa waliokuwa hapo.