-
Mashambulizi ya makombora ya wanamgambo wa RSF yaua takriban raia 21 katikati mwa Sudan
Sep 09, 2024 07:07Raia wasiopungua 21 wameuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa baada ya wanamgambo wa kikosi cha radiamali ya haraka (RSF) kuvurumisha makombora sokoni katika mji wa Sinnar katikati mwa Sudan.
-
Sudan yapinga ripoti ya Umoja wa Mataifa, yasema ni ya kisiasa
Sep 08, 2024 08:33Sudan imekadhibisha ripoti mpya ya Jopo Huru la Umoja wa Mataifa la Kutafuta Ukweli, ambayo inazituhumu pande zinazozozana nchini humo kwa kufanya ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu ambao unaweza kuwa uhalifu wa kivita.
-
Bwawa laporomoka na kuua watu zaidi ya 60 nchini Sudan
Aug 26, 2024 07:34Kwa akali watu 60 wameripotiwa kufariki dunia baada ya bwawa moja kuvunjika huko mashariki mwa Sudan kutokana na mvua kubwa inayoendelea kunyesha nchini humo.
-
Malori ya misaada yawasili Sudan baada ya kukwama kwa miezi kadhaa
Aug 22, 2024 08:31Msemaji wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa zaidi ya malori 12 kutoka mashirika ya misaada yamevuka mpaka na kuingia Sudan kupitia kivuko cha Adre katika mpaka na Chad ili kuleta misaada kwa ajili ya raia walioathiriwa na njaa katika jimbo la Darfur.
-
Sudan yatangaza janga la kipindupindu baada ya mvua kubwa kunyesha nchini humo
Aug 18, 2024 03:34Waziri wa Afya wa Sudan ametangaza janga la kipindupindu nchini humo baada ya mvua kubwa kunyesha kwa wiki kadhaa.
-
Udhalilishaji wa kingono watumiwa kama silaha ya vita katika mzozo huko Sudan
Aug 17, 2024 22:58Pande husika katika vita vya ndani nchini Sudan zimetekeleza udhalilishaji wa kingono na vitendo vingine vya unyanyasaji kama silaha ya vita tangu kuanza mapigano ya ndani nchini humo mwezi Aprili mwaka jana.
-
Waliokufa kutokana na mvua, mafuriko Sudan wapindukia 50
Aug 11, 2024 04:04Watu zaidi ya 50 wamefariki dunia na wengine zaidi ya 200 kujeruhiwa kutokana na mvua kubwa inayoendelea kunyesha na kusababisha mafuriko katika maeneo mbali mbali ya Sudan.
-
WHO: Vita vimefanya tuluthi 2 ya Wasudan washindwe kutafuta matibabu
Aug 09, 2024 03:48Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) amesema thuluthi mbili ya wananchi wote wa Sudan hawawezi kutafuta huduma za matibabu kutokana na mgogoro na vita vinavyoendelea kushuhudiwa nchini humo.
-
Mafuriko kaskazini mwa Sudan yaua na kujeruhi makumi ya watu
Aug 06, 2024 23:50Shirika rasmi la Habari la Sudan (SUNA) limeripoti kuwa watu 11 wamefariki dunia na wengine 60 kujeruhiwa kutokana na mvua kubwa iliyonyesha na kusababisha mafuriko katika mji wa Abu Hamad kaskazini mwa Sudan. Mvua hiyo imebomoa makumi ya nyumba huku timu za uokoaji zikiendelea kusaka watu waliotoweka na wengine walionasa chini ya vifusi.
-
FAO: Hatua za haraka zichukuliwe kukabiliana na njaa katika baadhi ya maeneo ya Darfur
Aug 05, 2024 23:26Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) limetoa wito wa kuchukuliwa hatua za haraka baada ya tatizo la njaa kuyaathiri baadhi ya maeneo ya Darfur. Shirika la FAO limeeleza haya katika ripoti yake ya karibuni kuhusu tathmini ya usalama wa chakula.