-
Mkuu wa jeshi la Sudan Abdel-Fattah al Burhan anusurika katika jaribio la mauaji
Jul 31, 2024 08:19Jeshi la Sudan limetangaza kuwa kamanda wake mkuu, Jenerali Abdel-Fattah al Burhan amenusurika katika shambulio la ndege mbili sisizo na rubani (droni) katika hafla ya wahitimu wa jeshi. Watu watano wameuawa katika hujuma hiyo ya droni mashariki mwa Sudan.
-
HRW: Pande hasimu Sudan zimeshiriki katika ukatili mkubwa wa kijinsia
Jul 29, 2024 22:59Pande zinazozozana huko Sudan zimeshiriki katika ukatili mkubwa wa kingono na kijinsia katika mji mkuu wa nchi hiyo, Khartoum.
-
Shambulio la RSF laua watu 22 el-Fasher, magharibi mwa Sudan
Jul 28, 2024 03:23Kwa akali watu 22 wameuawa katika shambulio linalodaiwa kufanywa na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) katika mji wa el-Fasher, jimboni Darfur, magharibi mwa Sudan.
-
Mvua kubwa yazidisha mateso ya wakimbizi mashariki mwa Sudan
Jul 27, 2024 03:32Mvua kubwa inayoendelea kunyesha huko mashariki mwa Sudan imezidisha mateso ya watu waliokimbia makazi yao haswa katika miji ya Gedaref, Kassala na Halfa Aj Jadeedah.
-
MSF: Theluthi moja ya waliojeruhiwa vitani huko Sudan ni wanawake au watoto wadogo
Jul 17, 2024 09:39Baada ya kupita zaidi ya mwaka mmoja wa vita vya wenyewe kwa wenyewe huko Sudan, karibu theluthi moja ya waliojeruhiwa ni wanawake au watoto walio na umri wa chini ya miaka 10. Ripoti hii imeelezwa na Shirika la Misaada ya Kimatibabu la Madaktari Wasio na Mipaka (MSF).
-
Jumanne, tarehe 9 Julai, 2024
Jul 08, 2024 22:51Leo ni Jumanne tarehe 3 Mfunguo Nne Muharram 1446 Hijria sawa na 09 Julai mwaka 2024.
-
Makundi ya kisiasa Sudan yakataa kutia saini taarifa ya mwisho ya mkutano wa Cairo
Jul 08, 2024 03:37Mkutano wa makundi ya kisiasa na kiraia ya Sudan ulimalizika jana mjini Cairo, Misri ambapo vyama vya Sudan vilijadili njia za kutatua mgogoro wa ndani wa nchi hiyo, huku baadhi ya makundi yakikataa kutia saini taarifa ya mwisho ya mkutano wa Cairo.
-
Shambulio la RSF laua watu 8 wa familia moja msikitini Sudan
Jul 02, 2024 02:40Watu wanane wa familia moja wameripotiwa kuuawa katika shambulio linalodaiwa kufanywa na wapiganaji wa kundi la Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) magharibi mwa Sudan.
-
Malik Agar: Kuporomoka kwa Sudan ni hatari kwa nchi zote za kanda hii
Jul 02, 2024 00:41Malik Agar, Makamu wa Rais wa Baraza la Utawala wa Sudan, ameonya juu ya hatari ya kuporomoka kwa Sudan, ambayo haitakuwa kwa nchi hiyo pekee, bali athari zake mbaya zitaenea katika nchi jirani na kwingineko.
-
Watu 755,000 wanakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula Sudan
Jun 28, 2024 00:22Wataalamu na maafisa wa ngazi za juu wa Umoja wa Mataifa wameonya kuwa, mapigano yanayoendelea nchini Sudan baina ya wanajeshi wa serikali na wanamgambo wa Vikosi vya Msaada wa Haraka RSF yatapelekea watu 755,000 kuwajihiwa na baa la njaa na uhaba mkubwa wa chakula katika miezi michache ijayo.