Feb 25, 2016 15:30
Muda wa kampeni za uchaguzi wa Bunge na Baraza la Wataalamu wanaomchagua Kiongozi Mkuu wa Iran umemalizika mapema leo saa mbili asubuhi tarehe 25 Februari na wananchi wa Iran kesho Ijumaa wataelekea kwenye masanduku ya kupigia kuwachagua wawakilishi wao katika zoezi litakaloanza asubuhi na kuendelea kwa masaa kumi.