-
Katika uamuzi wa aina yake.. Rais wa zamani wa Ufaransa ahukumiwa kifungo miaka 3 jela katika kesi ya ufisadi
May 17, 2023 07:39Mahakama ya Rufaa ya Paris leo, Jumatano, imemhukumu Rais wa zamani wa Ufaransa, Nicolas Sarkozy kifungo cha miaka 3 jela, ambapo anawekwa chini ya uangalizi kwa kufungwa bangili ya kielektroniki. Ni baada ya kupatikana na hatia ya kuhusika na ufisadi na kutumia vibaya madaraka, hatua ambayo haijawahi kushuhudiwa dhidi ya rais wa zamani wa Ufaransa.
-
Ombi la Ufaransa na Marekani kwa China kuitaka iwe msuluhishi katika vita vya Ukraine
Apr 07, 2023 04:49Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa siku ya Jumatano aliwasili Beijing kwa ziara ya siku tatu nchini China. Ziara hiyo ni ya kwanza kufanywa na Macron nchini China tangu mwaka 2019. Rais huyo wa Ufaransa jana alifanya mazungumzo na mwenyeji wake Rais Xi Jinping.
-
Burkina Faso yawafukuza wanahabari wa magazeti ya Ufaransa
Apr 02, 2023 23:52Serikali ya kijeshi ya Burkina Faso imewatimua nchini humo maripota wa magazeti ya Ufaransa ya 'Le Monde' na 'Libération' huo ukiwa ni muendelezo wa hatua za nchi hiyo Afrika Magharibi za kukabiliana na vyombo vya habari vya nchi hiyo ya Ulaya.
-
Burkina Faso yaifungia 'France 24' baada ya mahojiano na al-Qaeda
Mar 27, 2023 22:50Serikali ya kijeshi ya Burkina Faso imesimamisha matangazo ya kanali ya televisheni ya Ufaransa ya France 24, baada ya chombo hicho kurusha hewani mahojiano kiliyoyafanya na kiongozi wa kundi la kigaidi la al-Qaeda tawi la Kaskazini mwa Afrika AQIM.
-
Aliachwa akihangaika na kifo peke yake; Hasira zatanda Ufaransa baada ya kifo cha mwanafunzi mwenye asili ya Kiarabu
Mar 24, 2023 22:50Mitandao ya kijamii nchini Ufaransa imeshuhudia wimbi kubwa la hasira na ghadhabu baada ya kifo cha mwanafunzi mwenye asili ya Kiarabu ambaye alipatwa na mshtuko wa moyo, huku kukiwa na shutuma kwamba uongozi wa shule ulimwacha akikabilina na kifo peke yake bila ya kumpa huduma ya dharura.
-
"Adui wa Ulaya na mtiifu kwa Uislamu"... Wafaransa wamshambulia afisa aliyetetea haki za Waislamu
Mar 16, 2023 22:57Wanaharakati na wanasiasa wa Ufaransa wamemshambulia kwa maneno Mratibu wa Kamisheni ya Ulaya ya Kupambana na Chuki Dhidi ya Waislamu, Marion Lalisse, baada ya kuchapisha kipande cha video kwa lugha ya Kiarabu katika Siku ya Kimataifa ya Kupambana na Chuki Dhidi ya Uislamu, na kufikia hatua ya kumutaja kuwa ni "adui wa Ulaya na mtiifu kwa Uislamu."
-
Iran yakosoa undumakuwili wa Ufaransa juu ya suala la haki za binadamu
Mar 12, 2023 04:29Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani undumakuwili wa Ufaransa, ambayo kwa upande mmoja inajinadi kuwa mbeba bendera ya kutetea haki za binadamu, lakini kwa upande wa mwngine inakanyaga haki hizo kwa vitendo.
-
Waziri Mkuu wa Mali: Tuna ushahidi, Ufaransa inashirikiana na magaidi
Mar 08, 2023 03:07Waziri Mkuu wa Mali, Choguel Kokalla Maïga, amefichua - katika mahojiano maalumu na televisheni ya Al-Jazeera ya Qatar- kuwa Bamako ina taarifa sahihi na ushahidi kwamba baadhi ya magaidi waliko nchini Mali wamekuwa wakiwasiliana na Ufaransa.
-
Burkina Faso yavunja rasmi makubaliano ya kijeshi ya 1961 na Ufaransa
Mar 02, 2023 09:39Burkina Faso imevunja rasmi makubaliano ya kijeshi iliyosaini na Ufaransa mwaka 1961, wiki chache baada ya kumtaka mkoloni wake huyo wa zamani kuondoa vikosi vyake na balozi wake nchini humo.
-
Kuondoka vikosi vya Ufaransa katika nchi ya Burkina Faso
Feb 21, 2023 07:22Hatimaye vikosi vya Ufaransa vimeondoka nchini Burkina Faso na kuhitimisha uwepo wake katika nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika uliodumu kwa miaka 10.