-
Baada ya kutimuliwa Ufaransa, magaidi 160 waangamizwa Burkina Faso
Feb 21, 2023 04:01Magaidi wasipoungua 160 wameangamizwa katika operesheni ya jeshi la Burkina Faso katika eneo la Sahel, wakati huu ambapo mabaki ya askari vamizi wa Ufaransa wanaendelea kuondoka nchini humo.
-
Iran yamshambulia Macron kwa kukutana na wanaopinga Mapinduzi ya Kiislamu
Feb 18, 2023 06:49Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amemjia juu Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa kwa kukutana na 'shakhsia' wanaopinga mfumo wa uongozi na Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran tokeo mwaka 1979.
-
Polisi ya Ufaransa yakandamiza maandamano ya wananchi
Feb 12, 2023 23:04Askari polisi nchini Ufaransa wamewashambulia vibaya mamia ya maelfu ya watu walioshiriki maandamano ya kulalamikia sera za Rais Emmanuel Macron wa nchi hiyo, na hususan mageuzi tata ya pensheni yaliyotazamiwa kuanza kutekelezwa mwaka huu wa 2023.
-
Tathmini ya maandamano ya ‘watu mamilioni moja’ Ufaransa ya kupinga sera za serikali ya Macron
Feb 12, 2023 23:03Takribani watu milioni moja waliandamana siku ya Jumamosi nchini Ufaransa ikiwa ni mara ya nne wakipinga sera za serikali ya Rais Emmanuel Macron.
-
Iran yajibu uropokaji wa Macron, yamtaka azungumzie silaha za nyuklia za Israel
Feb 03, 2023 23:55Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amekosoa matamshi ghalati ya Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa aliyedai katika mazungumzo yake na Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel kuwa, eti Paris inatiwa wasiwasi na shughuli za nyuklia za Jamhuri ya Kiislamu.
-
Waziri: Migomo itatatiza usafiri wa umma kote nchini Ufaransa
Jan 29, 2023 23:16Waziri wa Uchukuzi wa Ufaransa amesema migomo ya wafanyakazi wa sekta hiyo kuanzia kesho Jumanne inatazamiwa kulemaza usafiri wa umma katika pembe zote za nchi hiyo ya Ulaya.
-
Kutangaza al-Azhar kususia bidhaa za Sweden na Uholanzi; ulazima wa kuchukua hatua kali dhidi ya kuvunjiwa heshima Qur'ani
Jan 26, 2023 00:33Jumatano ya jana tarehe 25 Januari Chuo cha Kiislamu cha al-Azhar cha nchini Misri kilitoa mwito kwa wananchi wa mataifa ya Kiarabu na Kiislamu kususia bidhaa za Uholanzi na Sweden kama moja ya njia za kuunga mkono Qur'ani Tukufu baada ya kushuhudiwa matukio mawili tofauti katika mataifa hayo ya kuchomwa moto Qu'ani Tukufu.
-
Ufaransa yatakiwa iondoe jeshi lake Burkina Faso haraka iwezekavyo
Jan 22, 2023 04:27Serikali ya kijeshi inayotawala Burkina Faso imeitaka Ufaransa iwaondoe wanajeshi wake katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi katika kipindi kifupi kijacho.
-
Wananchi wa Burkina Faso waandamana dhidi ya Ufaransa
Jan 21, 2023 06:48Mamia ya wananchi wa Burkina Faso wamejitokeza mabarabarani katika mji mkuu Ouagadougou kushiriki maandamano dhidi ya Ufaransa, hatua inayoonesha jinsi ushawishi wa Paris katika nchi za bara la Afrika unavyoendelea kupungua.
-
Afisa wa Ufaransa atahadharisha kuhusu hatari ya ujasusi wa Marekani barani Ulaya
Jan 15, 2023 23:40Mkuu wa Kamandi ya Ulinzi wa Kimtandao wa Ufaransa ametahadharisha kuhusu hatari ya ujasusi wa Marekani kwa bara Ulaya.