-
Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 8.7 laikumba pwani ya Russia, tahadhari ya Tsunami yatolewa
Jul 29, 2025 23:41Tahadhari za kuzuka Tsunami zimetolewa katika nchi kadhaa baada ya tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 8.7 kulikumba eneo la mashariki ya Russia la Peninsula ya Kamchatka.
-
UN: Israel imegeuza theluthi mbili za ardhi ya Ghaza kuwa eneo lisiloruhusiwa kufika
Apr 04, 2025 23:06Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA) imetangaza kuwa, hivi sasa utawala wa Kizayuni wa Israel umewawekea vizuizi Wapalestina vya kutoruhusiwa kufika kwenye takriban theluthi mbili ya eneo la Ukanda wa Ghaza, ama kwa kuyatangaza maeneo makubwa kadhaa ya ukanda huo kuwa ni marufuku kufika au kutoa amri ya kuwalazimisha wananchi hao kuyahama makazi yao.
-
Ufisadi Serikalini unawafanya vijana wengi wa Kiafrika wahajiri na kukimbilia Ughaibuni
Sep 03, 2024 23:09Karibu asilimia 60 ya vijana wa Kiafrika wanataka kuzihama nchi zao kwa sababu serikali zao hazishikiki kwa ufisadi. Hayo ni kwa mujibu wa uchunguzi mpya wa maoni uliofanywa kwa vijana katika mataifa 16 ya Afrika.
-
Watu 6 wauawa katika ufyatuaji risasi Las Vegas, Marekani
Jun 26, 2024 03:42Takriban watu 6 wameuawa kwa kupigwa risasi huko Las Vegas, Nevada, huko Marekani akiwemo mshukiwa.
-
Watu watatu wauawa kwa kupigwa risasi katika jimbo la North Carolina Marekani
Apr 30, 2024 03:51Watu watatu wameuawa katika ufyatuaj risasi uliotokea katika jimbo la North Carolina nchini Marekani.
-
13 wauawa, 21 wajeruhiwa katika shambulio la ufyatuaji risasi kwenye skuli moja ya Russia
Sep 26, 2022 07:32Polisi ya Russia imetangaza kuwa watu 13 wameuawa na wengine 21 wamejeruhiwa katika shambulio la ufyatuaji risasi lililotokea kwenye skuli moja kusini mwa nchi hiyo.
-
Kamala Harris akiri kuwepo silaha nyingi Marekani
Jul 19, 2022 03:33Makamu wa Rais wa Marekani amekiri kuwa, silaha zilizopo nchini humo ni nyingi zaidi ya watu wa nchi hiyo.
-
Maandamano makubwa kila pembe ya Marekani na mwito wa kuchukuliwa hatua kali zaidi za kudhibiti silaha moto
Jun 13, 2022 02:32Ongezeko kubwa la matukio ya ufyatuaji risasi dhidi ya halaiki nchini Marekani na kuongezeka pia idadi ya watu wanaouawa kwa mashambulio ya utumiaji wa silaha hizo kunakotokana na upuuzaji wa viongozi wa White House na mashinikizo ya lobi za watengezaji silaha, vimeibua wimbi kubwa la maandamano ya malalamiko ya raia wa nchi hiyo.
-
Mama ashtakiwa Marekani baada ya mtoto wa miaka 2 kumuua baba kwa kumpiga risasi
Jun 07, 2022 23:08Mwanamke mmoja katika mji wa Orlando jimboni Florida nchini Marekani ameshtakiwa kwa kosa la kumuua mumewe bila kukusudia baada ya mtoto wao wa miaka miwili kufyatua risasi kwa bahati mbaya ndani ya nyumba yao iliyompata mgongoni baba mtu na kumuua.
-
Kwa sababu ya chuki, kijana Mzungu awaua kwa kuwapiga risasi watu 10 mjini Buffalo, Marekani
May 14, 2022 23:02Katika mwendelezo wa vitendo vya ukatili wa mauaji ambavyo haviwezi kudhibitiwa tena nchini Marekani, kijana mmoja Mzungu mwenye umri wa miaka 18 amewaua kwa kuwapiga riasasi watu wasiopungua kumi na kuwajeruhi wengine watatu katika duka kuu moja la mji wa Buffalo, New York Marekani.