• Mamia ya wanaharakati wa Kiislamu wakamatwa Bangladesh kwa kupinga safari ya Modi

    Mamia ya wanaharakati wa Kiislamu wakamatwa Bangladesh kwa kupinga safari ya Modi

    Apr 19, 2021 13:30

    Polisi ya Bangladesh imewatia nguvuni mamia ya wanaharakati wa Kiislamu baada ya mandamano yaliyoandamana na umwagaji damu ya kupinga safari ya Waziri Mkuu wa India nchini humo mwishoni mwa mwezi Machi mwaka huu.

  • Mahakama Kuu ya India yatengua sheria ya marufuku ya kubadili dini

    Mahakama Kuu ya India yatengua sheria ya marufuku ya kubadili dini

    Apr 14, 2021 02:35

    Mahakama ya Juu ya India imetengua sheria inayowapiga marufuku raia wa nchi hiyo kubadili dini kutoka kwenye imanii ya Kihindu na kuingia kwenye Uislamu au ukristo. Taarifa iliyotolewa na mahakama hiyo imesema kuwa, sheria hiyo inapingana na katiba ya nchi.

  • Dunia yaendelea kukosoa azimio la Seneti ya Ufaransa kuhusu marufuku ya hijabu

    Dunia yaendelea kukosoa azimio la Seneti ya Ufaransa kuhusu marufuku ya hijabu

    Apr 11, 2021 03:36

    Watumiaji wa mitandao ya kijamii nchini Ufaransa na maeneo mengine ya dunia wameanzisha kampeni iliyopewa jina la Hands Off My Hijab (@handsoffmyhijab) wakieleza hasira zao dhidi ya azimio la Baraza la Seneti la Ufaransa la kuzidisha vizuizi na marufuku dhidi ya vazi la staha la mwanamke wa Kiislamu, Hijabu. Watu wengi wamesema kuwa azimio hilo linapiga vita Uislamu. 

  • Muslim Advocates yaitaka Facebook ikomeshe chuki dhidi ya Uislamu

    Muslim Advocates yaitaka Facebook ikomeshe chuki dhidi ya Uislamu

    Apr 10, 2021 02:35

    Taasisi ya Muslim Advocates imewasilisha mashtaka mahakamani dhidi ya Facebook, Mkurugenzi Mtendaji wake, Mark Zuckerberg na kiongozi nambari mbili wa kampuni hiyo, Sheryl Sandberg ikiitaka Facebook kutilia maanani harakati zinazoeneza chuki na uhasama dhidii ya Waislamu katika mtandao huo.

  • Jumuiya ya Wasomi wa Kiislamu yalaani ombi la Ufaransa la misikiti kubariki ndoa za mashoga

    Jumuiya ya Wasomi wa Kiislamu yalaani ombi la Ufaransa la misikiti kubariki ndoa za mashoga

    Mar 28, 2021 03:16

    Jumuiya ya Kimataifa ya Wanazuoni wa Kiislamu imelaani wito wa serikali ya Ufaransa iliyowataka maimamu wa misikiti nchini humo kubariki na kuhalalisha ndoa baina ya mashoga na watu wenye jinsia moja, ikisisitiza kuwa wito huo unaonyesha msimamo wa kindumakuwili dhidi ya Uislamu.

  • Kuendelea chuki za rais wa Ufaransa dhidi ya Uislamu

    Kuendelea chuki za rais wa Ufaransa dhidi ya Uislamu

    Nov 23, 2020 01:04

    Ikiwa ni kuendeleza chuki zake dhidi ya Uislamu na Waislamu, rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, sasa ametoa muhula maalumu kwa viongozi wa makundi ya Kiislamu ya nchi hiyo kuhakikisha wanajivika utamaduni wa Magharibi hata katika mambo ambayo ni haramu kwa mujibu wa mafundisho ya dini tukufu ya Kiislamu.

  • Erdogan: Dunia ipige vita uadui dhidi ya Uislamu sawa ilivyo katika suala la kupiga vita Uyahudi

    Erdogan: Dunia ipige vita uadui dhidi ya Uislamu sawa ilivyo katika suala la kupiga vita Uyahudi

    Nov 03, 2020 02:45

    Rais Recep Tayyip Erdoğan wa Uturuki ameitaka dunia ijifunze na kupata somo na ibra kutokana na uzembe wa jamii ya kimataifa iliyoacha kuzuia mauaji ya kimbari ya Waislamu wa Bosnia Herzegovina na kusisitiza kuwa, dunia inapaswa kupiga marufuku na kupambana na chuki na uhasama dhidi ya Uislamu kama ilivyopambana na chuki dhidi ya Uyahudi baada ya Holocaust (yanayodaiwa kuwa mauaji ya Mayahudi wakati wa Vita vya Pili vya Dunia).

  • Waziri Mkuu wa Canada apingana na Macron, asema Uislamu hauna mfungamano na ugaidi

    Waziri Mkuu wa Canada apingana na Macron, asema Uislamu hauna mfungamano na ugaidi

    Oct 30, 2020 08:54

    Waziri Mkuu wa Canada, Justin Trudeau amesema kuwa gaidi aliyetekeleza hujuma ya kigaidi katika mji wa Nice nchini Ufaransa hawakilishi dini ya Uislamu wala Waislamu, na kwamba watu wote wanapasa kukiri ukweli huo.

  • Radiamali ya kindumakuwili ya Ufaransa kufuatia malalamiko ya Waislamu duniani

    Radiamali ya kindumakuwili ya Ufaransa kufuatia malalamiko ya Waislamu duniani

    Oct 28, 2020 07:41

    Waislamu duniani kote wamekasirishwa na kushadidi vitendo vya chuki dhidi ya Uislamu nchini Ufaransa hasa cha kuchapishwa tena katuni zinazomvunjia heshima Mtume Muhammad SAW. Hasira za Waislamu zimeongezeka maradufu baada ya Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa kutetea vitendo hivyo vya chuki dhidi ya Uislamu kwa kisingizo cha uhuru wa maoni.

  • Pogba 'ajiuzulu' timu ya taifa ya Ufaransa kufuatia matamshi ya Macron dhidi ya Uislamu

    Pogba 'ajiuzulu' timu ya taifa ya Ufaransa kufuatia matamshi ya Macron dhidi ya Uislamu

    Oct 26, 2020 11:51

    Mchezaji nyota wa soka, Paul Pogba ameripotiwa kujiuzulu katika timu ya taifa ya soka ya Ufaransa, kutokana na matamshi yaliyotolewa na Rais Emmanuel Macron wa nchi hiyo ya Ulaya dhidi ya Uislamu, wakati akitetea vitendo vya kutusiwa na kuvunjiwa heshima Mtume Muhammad (SAW).