-
Kuongezeka upinzani dhidi ya vitendo vya kijinai vya utawala wa Kizayuni katika nchi za Magharibi
Nov 06, 2023 23:01Mwezi mmoja ukiwa umepita tangu kujiri operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa na utawala wa Kizayuni kuanzisha mashambulizi makali ya mabomu ambayo hajawahi kushuhudiwa tena huko Ghaza, ambayo yamepelekea kuuawa shahidi na kujeruhiwa makumi ya maelfu ya Wapalestina, wengi wao wakiwa ni watoto na wanawake, mwenendo wa upinzani dhidi ya vitendo hivyo vya jinai vya Israeli, umeongezeka sana duniani ikiwa ni pamoja na nchini Marekani, ambayo ni mwitifaki mkubwa wa Tel Aviv.
-
Jenerali Ashtiani: US itakabiliwa na pigo zito iwapo vita vya Gaza havitamalizika
Nov 05, 2023 23:29Waziri wa Ulinzi wa Iran ameonya kuwa, Marekani itakabiliwa na pigo kubwa na zito iwapo itashindwa kusimamisha mashambulizi ya kinyama yanayofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
UN: Zinahitajika dola bilioni 1.2 kukidhi mahitaji ya mamilioni Gaza, Ukingo wa Magharibi
Nov 03, 2023 23:34Ofisi ya Uratibu wa Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa (OCHA) imetangaza kuwa, takriban dola bilioni 1.2 zinahitajika kwa ajili ya kushughulikia mahitaji ya msingi ya Wapalestina milioni 2.7 katika Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
"Vita vya Israel dhidi ya Gaza vinafanana na vita vya Saddam dhidi ya Iran"
Nov 03, 2023 08:59Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema mashambulizi yasiyo na kikomo ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza yanashabihiana na vita vya kivamizi na kichokozi vya dikteta wa zamani wa Iraq, Saddam Hussein dhidi ya Iran katika miaka ya 1980.
-
Abdollahian: Jitihada za kusitisha vita Gaza kwa njia za kisiasa zinaendelea
Nov 01, 2023 23:29Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu na Qatar zinaendeleza juhudi za kisiasa za kutaka kusimamishwa vita kwa muda katika Ukanda wa Gaza haraka iwezekanavyo, huku utawala wa Kizayuni wa Israel ukiendelea kufanya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina katika eneo hilo lililozingirwa.
-
Abdollahian na Haniya wakutana Doha na kujadili matukio ya Ukanda wa Gaza
Nov 01, 2023 01:04Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS, ambapo wamebadilishana mawazo kuhusu matukio yanayoendelea kushuhudiwa katika Ukanda wa Gaza.
-
Shambulizi la Israel dhidi ya kambi ya wakimbizi Jabalia laua Wapalestina 200
Oct 31, 2023 12:06Mamia ya Wapalestina wameuawa shahidi katika shambulizi la utawala wa Kizayuni wa Israel lililolenga kambi ya wakimbizi ya Jabalia katika Ukanda wa Gaza.
-
Hatua mpya za Marekani katika fremu ya kuuunga mkono utawala wa Kizayuni wa Israel
Oct 30, 2023 08:05Tangu kuanza duru mpya ya vita kati ya utawala wa Kizayuni na makundi ya muqawama ya Palestina na operesheni ya Kimbunga ya Al-Aqsa na radiamali kali ya Wazayuni dhidi ya hatua hiyo, Marekani ikiwa mshirika wa kistratijia wa Israel imetoa himaya kubwa ya kisiasa, kidiplomasia na kijeshi kwa utawala huo ghasibu. Filihali Washington imechukua hatua mpya katika mwelekeo huu.
-
Pyongyang: Israel imefanya jinai ya kivita kwa kushambulia hospitali Gaza
Oct 26, 2023 23:00Korea Kaskazini imelaani vikali shambulio la anga lililofanywa na jeshi la utawala haramu wa Israel dhidi ya Hospitali ya Al Ahli Arab katika Ukanda wa Gaza mnamo Oktoba 17 na kuua mamia ya wananchi wa Paalestina.
-
Iran: Marekani ni mshirika wa jinai za Israel dhidi ya Wapalestina wa Gaza
Oct 25, 2023 04:07Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema Marekani ni mshirika katika jinai za kutisha za Israel huko Ukanda wa Gazal kutokana na uungaji mkono wake usio na kifani kwa utawala huo unaokalia kwa mabavu ardhi za Palestina.