-
Madai ya shambulio la kombora la Russia dhidi ya Poland: Njama za kuzusha mgogoro mpya wa Magharibi dhidi ya Moscow
Nov 16, 2022 22:48Wizara ya Mambo ya Nje ya Poland imetangaza kuwa: "Siku ya Jumanne alasiri, kombora la jeshi la Russia lilipiga kijiji cha "Przewodów" mashariki mwa Poland kilichoko umbali wa kilomita sita kutoka kwenye mpaka wa Ukraine, na kuua Wapoland wawili."
-
Marekani yaitaka Ukraine ifanye mazungumzo ya amani na Russia
Nov 14, 2022 07:12Maafisa wa ngazi za juu wa Marekani wameanzisha kampeni ya kuishawishi Ukraine itafakari juu ya suala la kufanya mazungumzo ya amani na Russia, wakihofia kuwa msimu wa baridi kali yumkini ukaikwamisha serikali ya Kiev baada ya eti kupata ushindi wa kulidhibiti tena eneo la Kherson.
-
Amir Abdollahian: Azimio la UN haliizuia Iran kuuza silaha nje ya nchi
Nov 12, 2022 04:40Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran amesema: "Kwa mujibu wa azimio nambari 2231 la Baraza la Usalama, hakuna marufuku ya kuagiza na kuuza silaha za Iran nje ya nchi, na Tehran haijaipa Russia silaha zozote ili zitumike katika vita vya Ukraine."
-
Abdollahian: Siasa za Iran za kukomeshwa vita vya Ukraine hazibadiliki
Nov 10, 2022 04:16Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, siasa za kimsingi na zisizobadilika za Jamhuri ya Kiislamu ni kuhitimishwa vita vya Ukraine.
-
Russia: Bado hatujaafiki rasmi kurefusha usafirishaji nje wa nafaka za Ukraine
Nov 09, 2022 03:47Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema kuwa, Moscow bado haijaamua rasmi kuafiki kurefushwa usafirishaji nje wa nafaka za Ukraine.
-
Onyo la Russia kuhusu Wamagharibi kutuma magaidi nchini Ukraine
Nov 04, 2022 08:45Katibu wa Baraza la Usalama wa Taifa la Russia, Nikolay Patrushev, ametangaza kuwa Marekani na Uingereza zinasajili na kuajiri magaidi wa kimataifa kwa ajili ya kushirikiana na jeshi la Ukraine katika vita dhidi ya Russia.
-
Italia yatangaza kusitisha kuipelekea silaha Ukraine
Nov 03, 2022 03:27Serikali ya Italia imetangaza kuwa imesitisha kuipelekea silaha Ukraine ambazo ilikuwa ikizipeleka huko kwa kisingizio cha kupambana na Russia na kutekeleza maazimio ya Jeshi la Nchi za Magharibi NATO.
-
Russia yaonya baada ya US kupeleka silaha mpya za nyuklia Ulaya
Oct 29, 2022 07:11Russia imekosoa vikali hatua ya Marekani ya kupeleka silaha mpya za kisasa za nyuklia za B61 katika kambi za Shirika la Kijeshi la Nchi za Magharibi (NATO) barani Ulaya na kuonya kuwa, ikilazimu, Moscow itatoa jibu kali kwa kitendo hicho.
-
Iran yaitaka Ukraine kutoathiriwa na baadhi ya wanasiasa wa Ulaya wenye misimamo mikali
Oct 29, 2022 00:52Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekanusha madai ya kutumika ndege zisizo na rubani za Iran katika vita vya Ukraine na kuitaka nchi hiyo kutoathiriwa na misimamo mikali ya baadhi ya wanasiasa wa Ulaya.
-
Mashtaka rasmi ya Russia kwa Umoja wa Mataifa kuhusu maabara za silaha za kibiolojia za Marekani nchini Ukraine
Oct 28, 2022 22:54Russia imepeleka malalamiko yake rasmi kwa Umoja wa Mataifa kuhusu kuwepo kwa maabara za silaha za kibiolojia za Marekani nchini Ukraine. Vasily Nebenzia, mwakilishi wa kudumu wa Russia katika Umoja wa Mataifa, amethibitisha kwamba nchi yake imekusanya ushahidi wa kutosha kuhusu uwepo wa maabara ya silaha hizo za kibiolojia za Marekani huko Ukraine.