-
UN: Wapalestina 400,000 Gaza wamefurushwa makwao ndani ya wiki 3
Apr 12, 2025 08:10Takwimu mpya za Umoja wa Mataifa zinaonyesha kuwa, idadi kubwa ya Wapalestina wamelazimika kuyahama makazi yao katika Ukanda wa Gaza tangu utawala haramu wa Israel uanzishe mashambulizi mapya baada ya kuvunja makubaliano ya usitishaji vita zaidi ya wiki tatu zilizopita.
-
UN: Mashambulio 36 ya Israel Ghaza kati ya Machi 18 hadi Aprili 9 yameua wanawake na watoto tu
Apr 11, 2025 23:38Umoja wa Mataifa umesema wanawake na watoto wa Kipalestina ndio pekee waliouawa katika mashambulizi yapatayo 36 ya anga yaliyofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Ghaza tangu katikati ya mwezi Machi na kuonya kwamba mashambulizi ya kijeshi ya Israel yanahatarisha "kuendelea kuwepo Wapalestina kama jamii".
-
UN: Katika kila nusu saa, mtoto 1 alibakwa mashariki ya DRC
Apr 11, 2025 22:49Umoja wa Mataifa umelaani kushtadi kesi za ubakaji na unyanyasaji wa kingono dhidi ya watoto huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zilizoripotiwa katika miezi miwili ya kwanza ya mwaka huu; huku makabiliano makali yakiendelea kati ya kundi la waasi la M23 na vikosi vya serikali.
-
Ripota wa UN: Muda wa kuwanusuru Wapalestina unazidi kuyoyoma
Apr 10, 2025 22:36Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya Palestina ameonya kwamba "hakuna muda mwingi uliobaki" kuwaokoa watu wa Palestina wakati huu ambapo Israel inaendeleza mashambulizi yake mtawalia katika Ukanda wa Gaza, na ukandamizaji unaoendelea katika Ukingo wa Magharibi.
-
Israel yaua Wapalestina wengine karibu 80 Gaza, Guterres asikitika
Apr 03, 2025 03:35Makumi ya Wapalestina wengine wameuawa shahidi katika mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel huko Gaza usiku kucha.
-
Mkuu wa UN atiwa wasiwasi na hali kuzidi kuwa tete Sudan Kusini
Mar 28, 2025 03:30Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres amesema anasikitishwa sana na kuendelea kushtadi taharuki na hali ya mambo nchini Sudan Kusini.
-
China yaitaka Syria iunde serikali shirikishi na ipambane na ugaidi
Mar 26, 2025 04:11Mwakilishi wa Kudumu wa China katika Umoja wa Mataifa amewataka viongozi wa mpito wa Syria waandae mchakato wa kuasisi serikali shirikishi na wachukua hatua madhubuti za kupabana na ugaidi nchini humo.
-
Makumi ya wafanyakazi wa UN wanaondoka Gaza, Israel yazidisha mauaji
Mar 25, 2025 23:11Kufuatia mashambulizi ya Israel dhidi ya kambi za Umoja wa Mataifa katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na kuuawa wafanyakazi watano wa shirika hilo la kimataifa, makumi ya wafanyakazi wa kimataifa wa Umoja wa Mataifa katika Ukanda wa Gaza wanaondoka eneo hilo kutokana na wasiwasi wa mashambulizi ya Israel.
-
UN, EU zataka kusitishwa vita Gaza huku Israel ikifanya mashambulizi mapya
Mar 22, 2025 01:02Umoja wa Mataifa na Umoja wa Ulaya zimetoa wito wa kusitishwa mara moja mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel huko Gaza, huku Israel ikianzisha tena vita vya mauaji ya kimbari kwenye ukanda huo.
-
Iran yakosoa vikali uingiliaji wa nchi za Magharibi katika kazi za Baraza la Haki za Kibinadamu UN
Mar 19, 2025 00:45Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Ofisi ya Umoja wa Mataifa mjini Geneva amezikosoa vikali baadhi ya nchi za Magharibi kwa kutumia vibaya taasisi za Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa na kusisitiza kuwa, nchi hizo zinataka kuingiza siasa katika masuala ya haki za binadamu dhidi ya Iran kwa kupuuza masuala ya kimsingi ya haki za binadamu ukiwemo mgogoro wa Palestina.