-
Guterres ahudhuria futari ya Waislamu Warohingya wa Myanmar kwenye kambi kubwa zaidi ya wakimbizi duniani
Mar 14, 2025 23:35Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amefuturu na wakimbizi wa Rohingya walioko kwenye kambi kubwa zaidi ya wakimbizi duniani, Cox Baazar nchini Bangladesh kuonyesha mshikamano na wakimbizi hao na wenyeji wanaowapa hifadhi.
-
UN: Wakati umefika wa kuunda serikali ya shirikishi nchini Syria
Mar 14, 2025 22:55Mwakilishi Maalumu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Syria amesisitiza kuwa, wakati umefika sasa wa kuchukua hatua za dhati na za kijasiri za kuunda serikali ya mpito na ya kuaminika nchini Syria.
-
UN yatoa wito wa kukomeshwa mauaji ya raia nchini Syria
Mar 10, 2025 03:29Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Turk ameonya katika taarifa yake kuhusu ghasia za hivi karibuni magharibi mwa Syria na kutoa wito wa kukomeshwa mauaji ya raia nchini humo.
-
Siku ya Wanawake; Iran yataka Israel itimuliwe UN + Picha
Mar 09, 2025 03:16Ofisi ya Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa imetaka utawala wa Kizayuni utimuliwe kutoka kwenye umoja huo kutokana na jinai kubwa unazofanya dhidi ya wananchi wa kawaida wa Palestina hasa wanawake na watoto wadogo.
-
Mjumbe wa UN ataka kuimarishwa hadhi ya wanawake nchini Libya
Mar 09, 2025 03:13Hanna Serwaa Tetteh, mwakilishi maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Libya ambaye pia ni mkuu wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo UNSMIL ametoa mwito wa kuinuliwa hadhi ya wanawake nchini Libya.
-
UN: Utawala wa Trump uache kuingilia uhuru wa mahakama
Mar 08, 2025 23:08Ripoti Maalumu wa Umoja wa Mataifa amekosoa vikali hatua za hivi majuzi za serikali ya Donald Trump ya kuwatimua na kuwateua maafisa wapya wa mahakama, akielezea wasiwasi wake kwamba hatua hizi ni sehemu ya vitisho kwa uhuru wa mfumo wa mahakama wa Marekani.
-
"Kutokomeza umaskini miongoni mwa wanawake kutachukua miaka 130"
Mar 08, 2025 03:30Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres ameashiria matatizo yanayoendelea kuwakabili wanawake na wasichana duniani kote, akionya kwamba "kutokomeza umaskini uliokithiri miongoni mwa wanawake na wasichana kutachukua miaka 130."
-
Elon Musk aunga mkono kujiondoa Marekani katika UN, NATO
Mar 02, 2025 08:55Bilionea Elon Musk ametangaza hadharani kuunga mkono wazo la Marekani kujiondoa kutoka Umoja wa Mataifa UN na Shirika la Kijeshi la Nchi za Magharibi NATO.
-
UN: Israel inakanyaga haki za binadamu Gaza, Ukingo wa Magharibi
Feb 27, 2025 07:31Mkuu wa Haki za Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa amesema utawala wa Israel umekuwa ukipuuza usio na kifani haki za binadamu" katika Ukanda wa Gaza, na kuitaja hali ya kibinadamu katika eneo hilo lililozingirwa kuwa "janga."
-
Iran yataka kuwepo uadilifu, kuheshimiana na amani ya kimataifa
Feb 26, 2025 03:11Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Ofisi za Umoja wa Mataifa mjini Geneva amesisitiza dhamira ya Jamhuri ya Kiislamu ya kuunga mkono ulimwengu wa pande kadhaa, sheria za kimataifa na kanuni za Mkataba wa Umoja wa Mataifa na kutoa wito wa kuwepo ulimwengu unaozingatia uadilifu, heshima na amani.