Aug 25, 2022 08:06
Edward "Ned" Price, msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani alisema jana Jumatano kuwa, Washington imetoa majibu kuhusu mitazamo ya Iran juu ya mazungumzo ya kuondolewa vikwazo Tehran. Amesema: Uchunguzi wetu kuhusu mitazamo ya Iran umekamilika na leo (Jumatano) tumekabidhi mapendekezo yetu kwa Umoja wa Ulaya.