May 18, 2022 03:04
Josep Borrell, Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya amesema katika mkutano wake na waandishi wa habari baada ya kikao cha mawaziri wa umoja huo mjini Brussels Ubelgiji kwamba, hakuna uwezekano wa kufikiwa makubaliano kuhusiana na kifurushi cha sita cha vikwazo dhidi ya Russia.