-
Wazayuni wapanga mashambulizi makubwa dhidi ya Msikiti wa Al-Aqsa wakati wa Pasaka
Feb 22, 2023 23:02Makundi na mashirika ya Kiyahudi yenye misimamo mikali yametoa wito kwa Wazayuni yakiwataka kuushambulia Msikiti wa Al-Aqsa katika mji unaokaliwa kwa mabavu wa Quds (Jerusalem) kwa mnasaba wa Pasaka ya Kiyahudi (Passover au Pesach).
-
Taarifa rasmi ya Baraza la Usalama ya kulaani vitongoji vya walowezi
Feb 21, 2023 23:02Jumatatu ya tarehe 20 Februari Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilipasisha rasimu ya azimio linalolaani uamuzi wa serikali ya Israel yenye misimamo ya kufurutu ada ya Benjamin Netanyahu wa kuidhinisha ujenzi wa vitongoji vipya tisa katika ardhi za Wapalestina za Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Wazayuni waliojifanya kusaidia wahanga wa matetemeko Uturuki kumbe ni wezi!
Feb 20, 2023 22:59Katibu Mkuu wa Harakati ya Ubunifu wa Kitaifa ya Palestina amefichua kuwa, timu ya utawala wa Kizayuni iliyojipeleka Uturuki kwa madai ya kusaidia wahanga wa mitetemeko ya ardhi, wameiba nyaraka za kihistoria ya Uturuki.
-
HAMAS yapongeza misimamo ya Umoja wa Afrika dhidi ya utawala haramu wa Israel
Feb 20, 2023 08:57Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imepongeza misimamo ya Umoja wa Afrika (AU) dhidi ya utawala haramu wa Israel na hatua yake ya kuliunga mkono taifa madhulumu la Palestina.
-
Iran: Mkutano wa usalama wa Munich umepoteza hadhi yake
Feb 20, 2023 08:25Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekosoa vikai mkutano wa usalama wa Munich na kubainisha kwamba, hatua zilizochukuliwa na waandaaji wa mkutano huo zimetoa pigo kubwa kwa itibari na hadhi ya mkutano huo wa usalama.
-
Faisal al-Miqdad: Shambulio la Israel kwenye maeneo ya raia ni uhalifu dhidi ya ubinadamu
Feb 20, 2023 04:11Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria amesema: "Shambulio la makombora lililofanywa Jumapili asubuhi na utawala wa Kizayuni wa Israel katika maeneo ya raia ya Damascus na vitongoji vyake ni jinai dhidi ya binadamu."
-
Wazayuni waliojipenyeza kilaghai kikao cha AU watimuliwa kidhalili na askari wa Afrika
Feb 18, 2023 22:57Ujumbe wa utawala waw Kizayuni ulioingia kilaghai katika kikao cha Umoja wa Afrika umetimuliwa kidhalili na kifedheha na askari wa Umoja wa Afrika.
-
Hamas yapongeza juhudi za Algeria na Afrika Kusini za kuifukuza Israel AU
Feb 16, 2023 04:27Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imepongeza juhudi zinazofanywa na nchi kama Afrika Kusini na Algeria za kuhakikisha utawala haramu wa Israel unapokonywa hadhi ya kuwa mwanachama mwangalizi katika Umoja wa Afrika (AU).
-
Msemaji wa Hamas: Muqawama, ngao na upanga vitaendelea kuwa mtetezi wa Palestina
Feb 13, 2023 22:58Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) amewapongeza wanamapambano wa Brigedi za Izzudin al Qassam kwa kukabiliana na chokochoko na mashambulizi ya karibuni ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Ghaza na kusisitiza kuwa, muqawama, ngao na upanga vitaendelea kuipigania Palestina.
-
Maandamano ya Wasudan ya kupinga kuanzishwa uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel
Feb 07, 2023 07:43Jumapili ya juzi tarehe 5 Februari wananchi wa Sudan waliandamana katika mji mkuu Khartoum kwa shabaha ya kupinga hatua ya utawala wa kijeshi nchini humo ya kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni wa Israel.