-
Jordan yatahadharisha dhidi ya Marekani kubadili msimamo kuhusu vitongoji vya utawala wa Kizayuni
Nov 19, 2019 23:00Waziri wa Mambo ya Nje wa Jordan Ayman Safadi ametahadharisha kitendo cha Marekani kubadili msimamo wake kuhusiana na ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni unaofanywa na utawala haramu wa Israel katika eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na kukitaja kitendo hicho kuwa hatari.
-
Hamas: Silaha za muqawama ndizo pekee zinazoitia hofu Israel
Nov 17, 2019 23:03Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema kuwa, silaha za muqawama ndizo pekee zinazodhamini usalama wa taifa la Palestina na kuilazimisha Israel ibaki kwenye makubaliano ya kusimamisha vita.
-
Wazayuni waendelea kushambulia Ghaza licha ya makubaliano ya kusitisha vita
Nov 16, 2019 04:22Ndege za kivita za utawala wa Kizayuni mapema leo asubuhi zimefanya mashambulizi mengine katika Ukanda wa Ghaza licha ya Israel yenyewe kuomba usitishaji vita na wanamuqawama wa Palestina.
-
Kiongozi: Kufutwa Israel maana yake ni wamiliki wa asili wa Palestina kuweza kuchagua serikali
Nov 15, 2019 10:23Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kufutwa Israel kuna maana ya kuondolewa utawala bandia wa Kizayuni na mahala pake kuchukuliwa na serikali iliyochaguliwa na wamiliki wa asili wa Palestina ambao ni Waislamu, Wakristo na Mayahudi.
-
Wanafunzi sita wa Palestina wauawa shahidi katika hujuma za utawala wa Kizayuni
Nov 15, 2019 10:21Wizara ya Elimu ya Palestina imetangaza kuwa, wanafunzi sita Wapalestina wameuawa shahidi kufuatia hujuma za hivi karibuni za utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Ghaza.
-
Wanamuqawama wa Palestina wasitisha vita baada ya Israel kukubali masharti yao
Nov 14, 2019 04:33Baada ya utawala haramu wa Kizayuni kukubali masharti ya wanamuqawama wa Palestina, makundi ya Kipalestina ikiwemo Harakati ya Jihadul-Islami yamekubali pendekezo la Misri kwa ajili ya kusimamisha vita.
-
Tawi la kijeshi la Jihadul-Islami lashambulia mkusanyiko wa askari wa utawala wa Kizayuni
Nov 13, 2019 04:39Wanamuqawama wa tawi la Al-Quds la Harakati ya Jihadul-Islami la Palestina, wameshambulia kwa kombora mkusanyiko wa askari wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel katika eneo la mashariki mwa Rafah.
-
Idadi ya askari wanaokimbia kuhudumu jeshini Israel yaongezeka
Nov 09, 2019 04:22Idadi ya askari wanaokimbia kuhudumu ndani ya jeshi la utawala haramu wa Kizayuni Israel, imezidi kuongezeka huku suala la matatizo ya kisaikolojia likitajwa kuwa ndio sababu.
-
Hamas yalaani nchi za Kiarabu zinazopigania kuwa na uhusiano na Israel
Oct 30, 2019 10:24Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, imezilaani nchi za Kiarabu ambazo zinapigania kuwa na uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel.
-
Harakati ya kimataifa ya kupinga mateso dhidi ya mateka wa Kipalestina yaanzishwa
Oct 24, 2019 23:20Zaidi ya taasisi na jumuiya 40 za Kipalestina na kimataifa zimeanzisha harakati ya kupinga mateso na unyanyasaji unaofanywa na maafisa wa utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya mateka wa Kipalestina wanaoshikiliwa katika jela na korokoro za utawala huo.