May 01, 2019 12:14
Jana Jumanne Caracas, mji mkuu wa Venezuela ulipitia siku ngumu na iliyojaa mitihani. Kwa mara nyingine Marekani na vibaraka wake wa ndani wanaoongozwa na Juan Guaido na ambao wanaendesha vurugu na upinzani dhidi ya serikali halali ya nchi hiyo walifanya jaribio la mapinduzi dhidi ya serikali ya mrengo wa kushoto inayoongozwa na Nicolas Maduro, kwa kushirikiana na baadhi ya wanajeshi, lakini kwa mara nyingine tena Marekani ikawa imeshindwa katika jaribio lake hilo la mapinduzi nchini Venezuela.