-
Mbunge wa chama cha Leba ataka sheria ya kuwaadhibu wanaomvunjia heshima Mtume (saw)
Jul 11, 2021 00:12Mbunge wa Uingereza ametetea heshima ya Mtume Muhammad (saw) katika hotuba ya kupendeza kwenye Bunge la nchi hiyo, akiangazia mashinikizo ya kiroho na madhara yaliyosababishwa kwa Waislamu ulimwenguni kote kutokana na katuni na picha zinazochapishwa mara kwa mara barani Ulaya zikimvunjia heshima Nabii huyo wa Mwenyezi Mungu.
-
Hilton kujenga hoteli kwenye magofu ya msikiti wa Waislamu wa Uyghur, Xinjiang; CAIR yalaani
Jul 07, 2021 01:25Mpango wa ujenzi wa hoteli ya kifahari ya Hilton kwenye eneo la msikiti wa Waislamu uliobomolewa katika mkoani Xinjiang nchini China umewakasirisha Waislamu na kuzusha malalamiko mengi katika nchi mbalimbali.
-
Mashirika 130 yataka Canada iache kuhujumu taasisi za Kiislamu
Jun 26, 2021 08:08Huku vitendo vya chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu vikionekana kushtadi nchini Canada, serikali ya nchi hiyo imekuja na mpango wa kuyafanyia 'ukaguzi' mashirika ya misaada ya kibinadamu ya Kiislamu nchini humo.
-
Waislamu Canada wahofishwa na kuongezeka mashambulio ya chuki dhidi yao
Jun 14, 2021 23:22Waislamu nchini Canada wamesema kuwa wana wasiwasi na kuongezeka mashambulizi na vitendo vya chuki dhidi yao.
-
Wapinzani wa utawala wa kijeshi Myanmar watangaza mshikamano na Waislamu wa Rohingya
Jun 14, 2021 03:47Wapinzani wa utawala wa kijeshi nchini Myanmar wameanzisha kampuni ya kuonyesha mshikamano wao na Waislamu wa jamii ya Rogingya wanaodhulumiwa na kukandamizwa nchini humo.
-
Maelfu waandamana kulaani 'Islamophobia' nchini Canada
Jun 12, 2021 08:40Maelfu ya watu wamefanya maandamano makubwa nchini Canada kulaani vitendo vya chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu, sambamba na kuonesha mshikamano wao na familia moja ya Kiislamu iliyouawa hivi karibuni katika mji wa London jimboni Ontario nchini humo.
-
Amnesty: China imewafanyia Waislamu wa Uighur 'jinai dhidi ya binadamu'
Jun 11, 2021 03:22Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limesema Waislamu wa jamii ya Uighur nchini China wanakabiliwa na vitendo vya mateso na unyanyasi unaoelezwa kuwa umekuwa ukifanywa na serikali ya Beijing, na kusisitiza kuwa dhulma hizo zina uzito wa 'jinai dhidi ya binadamu.'
-
Waislamu Burundi wamjia juu waziri aliyeivunjiwa heshima adhana
Jun 10, 2021 08:47Waislamu Nchini Burundi wamemkosoa vikali waziri mmoja nchini humo kwa kuivunjia heshima Adhana, ambao ni mwito kwa Waislamu kwenda kutekeleza ibada ya Swala, moja ya nguzo muhimu za dini hiyo tukufu.
-
Mauaji ya familia ya Kiislamu nchini Canada, nembo ya Islamophobia katika nchi za Magharibi
Jun 09, 2021 07:00Kufuatia mauaji ya kikatili ya familia moja ya Kiislamu kwenye mji wa London katika jimbo la Ontario nchini Canada, Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Justin Trudeau amesema anahidi kuwa, atachukua hatua zaidi za kukabiliana na makundi yenye misimamo mikali ya mrengo wa kulia.
-
Wanaharakati: UN itambue mauaji ya Mashia Afghanistan kuwa ni mauaji ya kimbari
May 19, 2021 22:05Wanaharakati wa haki za binadamu na utamaduni nchini Afghanistan wameutaka Umoja wa Mataifa utambue rasmi mauaji ya Waislamu wa madhehebu ya Shia nchini Afghanistan katika miaka ya hivi karibuni kuwa ni mauaji ya kimbari.